Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, February 1, 2010

MWAMUZI KATI YA MISRI NA ALGERIA AFUNGIWA NA CAF

Mwamuzi wa Benin Bonaventure Koffi Codjia amefungiwa na shirikisho la kandanda barani Afrika.
Hatua hiyo imekuja kufuatia kutomchukulia hatua yeyote golikipa wa timu ya taifa ya Algeria Fawzi Chaouchi, ambaye alimpiga kichwa katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya Misri.
Golikipa huyo alipewa kadi ya njano licha ya kufanya kosa hilo kubwa mchezoni.
Codjia, ambaye ni moja ya waamuzi ambao watachezesha michuano ya fainali za Dunia, hakuliandika kosa hilo la kupigwa kichwa na golikipa katika ripoti ya mchezo ambao Algeria walilala kwa magoli 4-0.
Golikipa Chaouchi katika mchezo huo baada ya kufungwa kwa goli la Penati alimkimbilia mwamuzi na kumgeuza mwamuzi Codjia na kumpiga kichwa huku akilalamikia penati hiyo.
Lakini baadae Chaouchi alitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumpiga kwanja mchezaji na kupewa kadi ya pili ya njano.
Caf imesema kamati ya nidhamu itasema baadae nini hatua zitachukuliwa kwa wachezaji Belhadj na Chaouchi hapo baadae.
Wachezaji hao wawili huenda wakakibiliwa na adhabu ya kufungiwa na kukosa fainali za Dunia.

No comments :

Post a Comment