Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, March 25, 2011

KAMPUNI YA SIMU YA ZANTEL YAPUNGUZA GHARAMA



KAMPUNI ya simu za mkononi ya Zantel wametambulisha viwango vipya vya kupiga simu vijulikanavyo kama ‘Umoja Tariff’ kuthibitisha viwango vyake ni bora na vya gharama nafuu sokoni. Viwango vya Umoja vinamwezesha mteja wa Zantel kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa TSH 2.50 kwa sekunde ikilinganishwa na TSH 3 kwa sekunde ya mitandao mingine. Pia wateja wa Zantel watafaidika zaidi na viwango hivi vya Umoja kwa kupiga simu kwa robo shilingi (TSH 0.25) Zantel kwenda Zantel kila siku kuanzia saa 5 usiku hadi saa 2 asubuhi.

Kaimu Meneja Masoko wa Zantel Bw.Brian Karokola,akizungumza na waandishi wa habari, alisema viwango hivi vipya alisema “Zantel inaheshimika kwa ubunifu na viwango na huduma zake zinazotumikia kila sehemu ya soko. Tunafahamu kuwa wateja wetu wanapendelea nini na kupitia viwango vya Umoja tumewapa wanachotaka ambacho ni thamani inayowawezesha kuongea kwa muda mrefu kwa gharama ndogo.” Viwango vya Umoja ni kwa wateja wa Dar es Salaam na Zanzibar pekee.

Wiki iliyopita Zantel walizinduwa viwango vipya vijulikanavyo kama Twanga Zaidi kwa wateja wake wa mikoani vinavyowawezesha wateja kupiga simu kwa robo shilingi Zantel kwenda Zantel masaa 24 na TSH 1.99 kwa sekunde kwenda mitandao mingine.

“Mtandao wa Zantel unajali wateja wake na kupitia viwango vyetu vipya tunakidhi mahitaji yao ambayo ni kuwawezesha kuwasiliana muda wowote kwa gharama nafuu na bila masharti.” Alimalizia Bw. Karokola.


No comments :

Post a Comment