Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, June 29, 2013

RECHO ANAAMINI


Na Elizabeth John


MWANADADA anayetamba katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini, Rachel Haule ‘Recho’, ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Niamini’ ambayo imeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio nchini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Recho alisema, anamshukuru Mungu nyimbo zake zinapokewa vizuri na mashabiki wake, hivyo anajitahidi kukamilisha video ya wimbo huo mwezi ujao ili kuwapa raha mashabiki wake.

“Muziki ni sehemu yangu ya kazi na sipendi mtu aidharau kazi yangu na sipendi kuwaudhi mashabiki wangu, ili kuepukana na hili nimeamua niwe natoa nyimbo ambazo zimeenda shule ili nisiwachoshe wapenzi wangu,” alisema Recho.

Recho, aliwaomba mashabiki wake wasikae mbali na yeye, kwani kuna vitu vingi amewaandalia ambavyo anaamini vitakuwa ni burudani kwao.

Licha ya kutamba na kibao hicho, Recho alishang’ara na nyimbo zake kama, ‘Upepo’, ‘Kizunguzungu’ ‘Nashikuru umerudi’ na nyinginezo

No comments :

Post a Comment