Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, November 4, 2013

REDDS MISS TANZANIA 2013 HAPPINESS WATIMANYWA AALIKWA NCHINI UGANDA KUSHIRIKI MAONYESHO YA MAVAZI.




 
Mrembo wa Taifa Redds Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa yuko Kampala Uganda kwa mwaliko rasmi kutoka kampuni ya Arapapa Fashion House & Design ya nchini Uganda.
 
Redds Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa atakuwepo nchini Uganda kwa muda wa siku 5 hadi tarehe 9 Novemba 2013 anatarajiwa kurejea nchini.
 
Akiwa nchini Uganda ataungana na warembo wengine kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Kenya, Rwanda, Burundi na wenyeji Uganda.
 
Pamoja na mambo mengine warembo hao watahusika pia katika kazi za jamii na baadaye kupanda jukwaani pamoja katika onyesho la mavazi lililoandaliwa na Kampuni hiyo.
 
Kampuni ya Arapapa imekuwa ikifuatilia kwa karibu mashindano ya urembo ya Miss Tanzania tangu mrembo Happiness  anyakue taji na waliazimia kumualika mrembo huyo kutembelea Uganda, jambo ambalo wamelitimiza.
 
Redds Miss Tanzania 2013 ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa  Shahada ya Juu katika Chuo cha Strathclyde  nchini Scotland, ameamua kuahirisha masomo yake kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi hapo atakapovua taji mwishoni mwa mwaka 2014.
 
Mrembo Happiness Watimanywa atawakilisha Tanzania katika mashindano ya urembo ya dunia hapo mwakani.

No comments :

Post a Comment