Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, November 20, 2013

RONALDO AIPELEKA URENO BRAZIL KWA HAT TRICK, UFARANSA NAYO YAFUZU




MSHAMBULIAJI wa Ureno, Cristiano Ronaldo ameipeleka timu yake katika fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil 2014 baada kufunga mabao matatu ‘hat trick’ katika ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Sweden.
Mchezo huo ambao uliwakutanisha mastaa wawili ambao ni manahodha wa timu hizo, Ronaldo anayeichezea Real Madrid na Zlatan Ibrahimovic anayekipiga katika timu ya PSG ya Ufaransa wote walikuwa wanawania nafasi ya kucheza fainali hizo pamoja na timu zao.
Ronaldo ambaye ndiye mfungaji wa bao la pekee katika mchezo wa kwanza uliochezwa wiki iliyopita nchini Ureno, alifunga bao la kwanza dakika ya 50 kabla ya Ibrahimovic kusawazisha dakika ya 68.
Ibrahimovic aliongeza bao la pili dakika ya 72 lakini dakika tano baadaye Ronaldo alimaliza matumaini ya Sweden kucheza fainali hizo mwakani baada ya kufua bao la pili. 

Wakati Sweden wakisaka bao la kuongoza ili wafufue matumaini ya kucheza fainali hizo, Ronaldo alizima kabisa ndoto hizo baada ya kupachika bao la tatu dakika ya 79 na kufanya mchezo huo umalizike kwa jumla ya mabao 4-2.
Nayo ufaransa imefanikiwa kutinga katika fainali hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 katika mchezo wake dhidi ya Ukraine shukrani mabao ya Mamadou Sakho dakika ya 22, Karim Benzema dakika ya 34 na bao la kujifunga na Oleg Gusev dakika ya 72. 


Timu nyingine zilizofanikiwa kutinga katika fainali hizo ni Ugiriki ambayo ilitoka sare na Romania ya mabao 1-1 lakini imefuzu kwa jumla ya mabao 4-2, wakati Croatia nayo wamepenya katika hatua hiyo baada ya kuifumua Iceland mabao 2-0.

No comments :

Post a Comment