Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, November 1, 2013

Yanga sasa 'chinjachinja' yaua tena maafande Taifa, Ngassa huyooo!




 Mshambulijia wa Yanga, Hamis Kiiza akiwa katika harakati za kufunga.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia.
Beki wa JKT Ruvu akiokoa moja ya hatari langoni mwake.
Kiungo wa JKT Ruvu, Nashon Naftal akimtoka Mrisho Ngasa.
Simon Msuva akichuana na Kessy Mapande wa JKT Ruvu.
Mashabiki wa Yanga wakishangilia timu yao.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao la tatu lililofungwa na Oscar Joshua. (Picha zote: Francis Dande)
JANGWANI wanacheka! Ndivyo unavyoweza kusema kutokana na Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga kuendelea kutoa dozi kwa timu za majeshi baada ya jioni hii kuivurumusha JKT Ruvu kwa mabao 4-0 na kukalia kiti cha uongozi wa ligi hiyo.
Mabao mawili ya mapema ya Mrisho Ngassa 'Uncle' na mengine ya kipindi cha pili yaliyofungwa na beki wa kushoto, Oscar Joshua na jingine la Jerry Tegete yameifanya Yanga kufikisha pointi 25 kutokana na kucheza mechi 12, huku Ngassa akifikisha jumla ya mabao matano katika orodha ya wafungaji na Tegete kufikisha manne.
Ushindi huo wa Yanga ni wa tatu mfululizo kwa maafande wa Jeshi baada ya awali kuitafuna Mgambo mabao 3-0 kisha kuisulubu Rhino Rangers kwa idadi kaka hiyo kabla ya leo kuisasambua JKT Ruvu.
Mabingwa hao watetezi watamaliza mechi zao za duru la kwanza kwa kuvaana tena na maafande wengine Oljoro JKT pambano lityakalochezwa Alhamis ijayo kwenye uwanja wa Taifa.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena wikiendi hii katika viwanja viwanja vitano kuamliza mechi za raundi ya 12 kabla ya Jumatano na Alhamis kuhitimishwa kwa ligi hiyo ambayo msimu huu imekuwa na msisimko na ushindani mkubwa.


Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014                                         P    W   D   L    F    A   GD  PTS
01. Yanga                   12    7    4    1   28  11   17    25
02. Azam                    11    6    5    0   17   7    10    23
03. Mbeya City           11    6    5    0   15   7     8     23
04. Simba                   12    5    6    1   22  11    11    21
05. Kagera Sugar        12    4    5    3   12    9    3     17
06. Ruvu Shooting       11    4    4    3   13   10   3     16
07. Mtibwa Sugar        11    4    4    3   16  15    1     16
08. Coastal Union        11    3    6     2   10   6    4     15
09. JKT Ruvu              12    4    0    8    9   16  -7     12
10.Rhino Rangers         11    2    4    5    9   15  -6     10
11.Ashanti                    11    2    4    5    10  19 -9     10
12.Prisons                    11    1    5    5     5   14 -9      8
13.Oljoro                     11    1    4    6     8    16 -8     7
14.Mgambo                 11    1    2    8     3    21 -18   5

Wafungaji:
9- Tambwe Amisi (Simba)
8- Hamis Kiiza (Yanga)
7- Elias Maguri (Ruvu Shooting), Juma Luizio (Mtibwa Sugar)
6- Kipre Tchetche (Azam)
5- Tumba Sued (Ashanti Utd), Themi Felix (Kagera), Didier Kavumbagu, Mrisho Ngassa (Yanga)
4-Peter Michael (Prisons), Jerry Santo (Coastal Union), Jerry Tegete (Yanga)
3- Haruna Chanongo, Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Themi Felix (Kagera), Paul Nonga (Mbeya City), Salum Machaku (JKT Ruvu), Jerry Santo (Coastal Union),
2- Haruna Moshi, Crispian Odulla (Coastal Union), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Mwagani Yeya, Jeremiah John, Peter Mapunda,(Mbeya City), Godfrey Wambura (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary (JKT Oljoro), Khamis Mcha (Azam), Shaaban Nditti (Mtibwa Sugar), Betram Mombeki, Ramadhani Singano (Simba), Said Dilunga (Ruvu Shooting)
1- Abdi Banda, Danny Lyanga (Coastal Union), Henry Joseph, Joseph Owino, Gilbert Kazze (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva, Frank Dumayo, Mbuyi Twitte, Oscar Joshua (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku, Kamana Salum, Hussein Abdallah, Abbas Mohammed (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah,  Aggrey Morris,  John Bocco, Joseph Kimwaga, Faridi Maliki, Hamphrey Mieno, Salum Abubakar, Erasto Nyoni (Azam), Steven Mazanda, Richard Peter, Deo Deus  (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Shaaban Susan, Jerome Lembeli, Cosmas Ader  (Ruvu Shooting), Masoud Ally, Shaaban Kisiga (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu, Paul Maono(OG), John Matei, Mwinyi Ally (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Clement Douglas, Salum Kanoni (Kagera Sugar), Paul Malipesa, Expedito Kidulo, Nurdin Mohammed, Fikiri Mohammed (Oljoro JKT)

No comments :

Post a Comment