Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, February 6, 2014

NAIBU WAZIRI KITWANGA APOKEA SHEHENA YA MWISHO YA MABOMBA YA MWISHO KATIKA BANDARI YA MTWARA




 Naibu Waziri Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Mhe. Charles Kitwanga (wa tatu kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na Menjeja wa Bandari ya Mtwara (wa pili kutoka kushoto) Bw. Absalim Bohella. Anayefuatia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Wilman Kapenjama Ndile, na uongozi wa Mkoa mara baada ya kupokea Shehena ya mwisho ya Mabomba ya Gesi katika bandari ya Mtwara.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Bandari ya Mtwara wakiendelea na kazi ya kupakua shehena ya mabomba ya gesi kutoka katika meli baada ya mabomba hayo kuwasili katika Bandari ya Mtwara.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Bandari ya Mtwara wakiendelea na kazi ya kupakua shehena ya mabomba ya gesi kutoka katika meli baada ya mabomba hayo kuwasili katika Bandari ya Mtwara.
 Mtaalamu wa Masuala ya Gesi na Msimamizi Mkuu wa Mitambo ya Kusafisha Gesi Mhandisi Sultan Pwaga (katikati) akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Charles Kitwanga na ujumbe wake alipotembelea eneo hilo kuangalia namna shughuli mbalimbali zinavyoendelea katika eneo hilo.
Naibu Waziri Mhe. Charles Kitwanga (wa pili kutoka kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Wilman Kapenjama Ndile, (wa kwanza kulia) wakipata  maelezo kutoka kwa mtaalamu Abshakim Marunda kuhusu namna kisima cha gesi cha nchi Kavu kinavyofanya kazi. Kwa mujibu wa Maelezo ya Mjiologia Mwandamizi wa TPDC Bw.George Ngwale hayupo pichani ameeleza kuwa, Mnazi Bay ina jumla ya visima vitano kati ya hivyo visima vine vina gesi inayochimbwa na kisima kimoja kikavu. Aidha gesi inayopatikana katika eneo hili inauzwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ambao wanatumia kuzalisha umeme unaosambazwa katika Mikoa ya Lindi na Mtwara. Wa kwanza kushoto ni Katibu wa Mhe. Naibu Waziri Bw. Mjengwa Ngereja.

=========  =========

 ==========  ========  ========
NAIBU WAZIRI CHARLES KITWANGA APOKEA SHEHENA YA MWISHO YA MABOMBA YA GESI
Na Asteria Muhozya, Mtwara
Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Mhe. Charles Kitwanga, amepokea Shehena ya mwisho ya mabomba ya gesi katika bandari ya Mtwara na kueleza kuwa, ujio wa miundo mbinu hiyo ni neema kwa uchumi wa Tanzania.
Aliongeza kuwa, hiyo ni hatua kubwa katika kufikia malengo tarajiwa ikizingatiwa kwamba, kukamilika kwa mradi huo kutachochea na kufungua njia mbalimbali za uchumi unaoendana na sekta ya gesi na mafuta.
“Ujenzi wa miundombinu ya kusafirisha gesi ni jambo jema kwa Tanzania, tunataka kuingia katika uchumi wa kati wa dola elfu tatu au karibu ya hapo, tunataka pato la mtanzania liongezeke. Sasa bila kuwa na umeme haya yote hatutayafikia. Gesi itazalisha mengi, tunataka tufikie lengo letu. Alisema.’’ Mhe. Kitwanga.
Aidha, aliongeza kuwa, kuzalishwa kwa gesi  na kusambazwa katika maeneo mbalimbali chini kutasaidia kufungua fursa nyingi ikiwemo  kuongezeka kwa viwanda ambavyo vitakuwa na uhakika  wa kupata umeme unaotokana na gesi.
Vilevile, alieleza kuwa, mbali na matumizi ya viwandani gesi inatarajiwa kutumiwa katika mahitataji mbalimbali yakiwemo matumizi ya majumbani.
 “Nataka kuwaeleza wana Mtwara, si kwamba gesi itachukuliwa yote, hapana. Tunachotaka kufanya ni kuisambaza maeneo mbalimbali lengo letu ni kukuza uchumi wetu kwa kutumia gesi hata Mtwara viwanda vitajengwa na fursa mbalimbali zitakuwepo”. Alisema.
Akieleza mafanikio ambayo yamekuwepo kutokana na shughuli za gesi kutumia bandari ya Mtwara, Meneja wa Bandari Bw. Absalim Bohella alieleza kuwa, ujio wa gesi na mradi unaotekelezwa Mkoani humo umekuwa neema kwa bandari hiyo kutokana na kuongezeka kwa mapato yanayotokana na bandari hiyo pia  kutumiwa kwa shughuli mbalimbali za gesi.
Aliongeza kuwa, tayari bandari ya Mtwara imevuka malengo ya ukusanyaji mapato waliojiwekea ambapo hadi sasa tayari zaidi ya Tsh. Milioni mia tano kimekusanywa.
Aidha, aliongeza kuwa, mradi wa gesi umewaongezea watumishi wa bandari hiyo ujuzi kutokana kufanya shughuli tofauti tofauti zinazohusiana na gesi ikiwemo upakuaji wa bidhaa zinazopitia katika bandari hiyo kwa shughuli.
“Bandari bila rasilimali watu si kitu. Kwa wafanyakazi waliobobea wamepata ujuzi zaidi na sasa wanao uwezo wa kuhudumia shughuli zote za bandari”. Aliongeza.
Akielezea hatua mbalimbali ambazo zimefikiwa katika ujenzi wa miundombinu ya gesi, Mtaalamu wa Masuala ya Gesi na Msimamizi Mkuu wa Mitambo ya Kusafisha Gesi Mhandisi Sultan Pwaga alieleza kuwa, shughuli za uwekaji mabomba ya gesi unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Julai, 2014 ambapo pia inatarajiwa mwanzoni mwa mwezi Disemba mwaka huu shughuli za usimikaji mitambo utakamilika.
 Vile vile, ameongeza kuwa, shehena hiyo iliyopokelewa katika bandari ya Mtwara ni ya mwisho lakini mabomba ya mwisho ya mradi yatapokelewa tarehe 10 Februari, 2014 katika bandari ya Dar es Salaam.
Aidha, aliongeza kuwa, miundombinu hiyo ndio kichocheo cha gesi asilia na lengo la mradi huo ni kuhakikisha kuwa, mitambo inajengwa mahali ambapo gesi asilia inachimbwa.
Mbali ya kupokea Shehena za mabomba ya mwisho ya gesi, Mhe. Kitwanga ametembelea eneo la Mnazi Bay ambako gesi asilia na kuuzwa katika Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ambapo shirika hilo linaitumia gesi hiyo kuzalisha umeme kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara.
Vilevile, Mhe. Kitwanga alitembelea katika eneo la Madimba kunakojengwa kambi za wafanyakazi na panapotarajiwa kujengwa mitambo ya kusafisha gesi.

No comments :

Post a Comment