Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, February 10, 2014

WanaCUF watakiwa kutovunjika moyo na matokeo ya uchaguzi mdogo jimbo la Kiembesamaki






Na Khamis Haji , OMKR

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amewataka wanachama na viongozi wa chama hicho wasivunjike moyo na matokeo ya uchaguzi mdogo wa jimbo la Kiembesamaki na badala yake waendelee na juhudi za kukiimarisha chama, ili kiweze kukamata dola katika uchaguzi mkuu wa mwakani.
Akifungua mkutano wa viongozi wa matawi, majimbo na Wilaya kwa Wilaya za Wete na Micheweni uliofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete, Maalim Seif amesema kilichotangazwa Kiembesamaki si matakwa ya wananchi, kwa vile  kimsingi wananchi wa jimbo hilo walisusia uchaguzi huo.
Maalim Seif amesema idadi kubwa ya wapiga kura walioshiriki katika uchaguzi huo si wakaazi wa eneo hilo, ambao walichukuliwa katika maeneo mbali mbali, baada ya kubainika wananchi wenyewe hawatashiriki kwa sababu hawakuridhishwa na maamuzi yaliyochukuliwa hadi kufanyika uchaguzi huo.
“Kama kuna wananchi wa Kiembesamaki waliokwenda kupiga kura basi hawazidi 1000, wengi walichukuliwa katika maeneo tafauti, kama vile Makunduchi, Mtende, Kitope na Bumbwini na wakapelekwa kupiga kura huku wakilindwa na vikosi vya Serikali”, alisema Maalim Seif.

No comments :

Post a Comment