Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, February 15, 2014

Simba yadroo, Coastal yakaa Mlandizi



* Mtibwa Sugar nayo yanyukwa nyumbani, kwingine sare tupu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhSNduSo1My318-j2v3bKrrs1t1Y99Z_U2FqDpdixeTYZspXf7ugGetaIEkIG4wEKfonAlXo0P-LCFXHvIG5x5C_v1DD6d7dx5Dq6VY4bmslcXpdFZiGXamcwoaqhQD9YLIguG4Z6UYdoF5/s1600/Simba+Vs+Mbeya+City.jpg
Deo Julius wa Mbeya na Haruna Chanongo wa Simba leo wote wamehusika na mabao ya jijini Mbeya. Hii ni mechi yao ya kwanza iliyoisha kwa sare ya 2-2

VIJANA wa Msimbazi, Simba jioni ya leo imeigomea Mbeya City nyumbani kwao kukweka kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuchomoa bao na kulazimisha sareya 1-1 katika pambano kali lililochezwa kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
Wakati Simba ikilazimisha sareugenini, Mtibwa Sugar imejikuta ikichezea kichapo toka kwa Prisons ya Mbeya, huku Mgambo JKT na  Rhino Rangers zikitoka sare ya 1-1 kama ilivyokuwa kwa Oljoro JKT dhidi ya JKT Ruvu na Coastal Union ikishindwa kuonyesha makali wa Oman kwa kulala kwa Ruvu Shooting.
Katika pambano la Mbeya, Simba walishtukizwa na bao la penati katika dakika 13 baada ya William Lucian 'Gallas' kunawa mpira  langoni mwake na Deogratius Julius kukwamisha na kudumu hadi wakati wa mapumziko licha ya kosa kosa za hapa na pale toka kwa timu zote.
Dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, Amissi Tambwe aliisawazishia Simba bao kwa kichwa na kuwa goli lake la 15 la mshambuliaji huyo kutoka Burundi baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Haruna Chanongo aliyepiga krosi murua.
Timu ziliendelea kushambuliana na kufanya mabadiliko ya wachezaji, lakini hakuna kitu kilichobadilika na kufanya mechi kuisha kwa sare ya 1-1 na timu hizo kugawa pointi moja moja na kuiacha Simba ikibakia nafasi ya nne ikiwa na pointi 32 na Mbeya ikifikisha pointi 35 na kulingana na Yanga, lakini uwiano wa mabao umeifanya kubaki nafasi ya tatu.
Kwa sare hiyo imeikwamisha Mbeya City kukwea kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo nafasi waliyokuwa nayo katika mchezo huo kwani ingefikisha pointi 37 na kuzishinda Azam na Yanga ambao wikiendi hii wana majukumu ya kimataifa ugenini nchini Comoro na Msumbiji.
Katika mechi nyingine, Mgambo JKT ilishindwa kuendeleza ubabe katika ligi hiyo baada ya kufungana bao 1-1 na Rhino Rangers mjini Tabora. Wenyeji walianza kuandika bao dakika ya 29 kupitia Gideon Mlami na Mgambo kusawazisha kipindi cha pili dakika ya 51 na Ajali Boli. huku Oljoro JKT kubanwa  nyumbani jijini Arusha mbele ya JKT Ruvu kwa kutoka 0-0 nayo Coastal Union ikisulubiwa na Ruvu Shooting Mlandizi-Pwani kwa kulazwa bao 1-0, bao lililofungwa na Said Dilunga.
Nao Ashanti United ikiwa uwanja wa nyumbani wa Chamazi, wakilazimishwa sare na Kagera Sugar ya kutofunga bao lolote, huku Mtibwa Sugar ikiwa uwanja wa Manungu imelazwa  bao 1-0 na wageni wao Prisons ya Mbeya.

No comments :

Post a Comment