Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, February 24, 2014

Nyamwela afyatua mpya na Tundaman



MNENGUAJI kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Mussa Hassan 'Super Nyamwela' amefyatua wimbo mpya uitwao 'Nyengele' akimshirikisha nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Tundaman ikiwa ni maandalizi yake ya kupakua albamu yake mpya na ya tatu.
Akizungumza na MICHARAZO, Super Nyamwela alisema wimbo huo ambao ni wa nne katika maandalizi ya albamu hiyo baada ya 'Duvele Duvele', na Maneno Maneno ameurekodia katika studio za C9 Records na anatarajia kuachia wiki ijayo.
Nyamwela alisema katika wimbo huo kama ulivyo 'Duvele Duvele' na 'Tumechete'  umepigwa kiasili kwa ajili ya kuleta vionjo tofauti na kutamba kuwa utakuwa funika bovu kwa namna Tundaman alivyompiga tafu.
"Nipo katika maandalizi ya mwisho ya kuachia audio na video ya wimbo wangu mpya uitwao 'Nyengele' ambao nimeuimba na Tundaman ikiwa ni maandalizi kutoa albamu yangu ya tatu baada ya 'Master of the Tample' na 'Afrika Kilomondo', " alisema Nyamwela.
Nyamwela alisema amepanga ndani ya mwaka huu albamu hiyo ya tatu itakuwa imekamilika na pia itafanyiwa uzinduzi , japo hajajua itafanyika mwezi gani na ukumbi gani.
"Nataka nikamilishe nyimbo zote audio na video kabla ya kuizindua rasmi," alisema Nyawela.

No comments :

Post a Comment