Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, September 5, 2014

Coastal Union kutambulisha wapya Coastal Day


http://www.gushit.com/files/bookmark_photos/29e2087425L.jpg

KLABU ya Coastal Union ya Tanga kesho inatarajiwa kutambulisha wachezaji wote waliosajiliwa kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara unaotazamiwa kuanza Septemba 20 mwaka huu.

Utambulisho huo utafanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga katika siku maalum ya Coastal 'Coastal Union Day' ambayo hufanyika kila mwaka inapofika Septemba 7.
Katika utambulisho huo Coastal maarufu kama Wagosi wa Kaya wataumana na timu iliyorejea Ligi Kuu Polisi Morogoro.
Ofisa Habari wa Coastal Union, Oscar Assenga amesema kuwa maandalizi ya kuelekea utambulisho huo yamekamilikwa kwa asilimia kubwa.

Assenga amesema katika kuelekea siku hiyo maalumu kwa timu hiyo wataangalia uwezekano wa kucheza na timu itakayotajwa baadae baada ya mazungumzo kumalizika.

"Siku hii itakuwa ni maalumu sana kwa timu yetu tunatarajia tutaweza kufanya jambo hilo kwa wanachama,wapenzi na mashabiki wetu ili waweze kufahamu kikosi chao kabla ya kuanza msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara"

Akizungumzia maandalizi ya kuelekea msimu mpya wa ligi kuu, Assenga amesema kuwa maandalizi kwa timu hiyo yanaendelea vizuri kwa wachezaji kufanya mazoezi asubuhi na jioni.

No comments :

Post a Comment