Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, December 29, 2012

UBUNGO BUS TERMINAL KUHAMA JANUARY 15, 2013.



MCHAKATO wa kuhamisha Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi (UBT), kwenda Mbezi Luis unatarajiwa kuanza Januari 15 mwaka ujao.
 
Akizungumzana wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Jiji Mussa Zungiza, alisema lengo la kuhamisha kituo hicho ni kwa ajili ya kupisha Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART).
 
Alisema kuhamishwa kwa kituo hicho kutakuwa kwa awamu, kutakakokwenda sambamba na kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho cha Mbezi.
 
“Siyo kweli kama ifikapo Januari tunahamisha au tunasimamisha shughuli zote pale Ubungo la hasha, tutakacho fanya pale tutawakabidhi wajenzi wa mradi huo wa DART ambao nao watachagua maeneo maalumu ya kuanzia shughuli zao, huku maeneo mengine yakiendelea kutoa huduma bila ya kuleta athari katika utoaji huduma”alisema Zungiza.
 
Zungiza alisema hadi sasa pale Mbezi kinachofanyika usafishaji wa eneo hilo la stendi hiyo mpya. Alisema katika awamu hiyo ya kwanza watejenga miundombinu ikiwemo uzio, alama za kuelekeza magari, njia za kuingia na kutoka.
 
“Pengine tunatarajia ndani ya miezi mitano tunaamini awamu yakwanza itakuwa imekamilika”alisema.
 
Zungiza alisema uhamishaji kabisa wa kituo hicho cha Ubungo kutategemea kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho kipya cha Mbezi. 

No comments :

Post a Comment