Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, May 18, 2014

TASWA FC 'KUSHINE' NA UZI MPYA WA RANGERS BUREAU DE CHANGE



 Mkurugenzi wa Rangers Bureau De Change na Rangers Tours and Travel Agent, Daudi Madega (kushoto) akikabidhi jezi kwa mwenyekiti wa Taswa FC,  Majuto Omary katika hafla fupi iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo, Magomeni.
Nahodha wa timu ya soka ya wandishi wa habari za michezo nchini, Mbozi Katala akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo.
Na Mwandishi Wetu, Dar
Duka la kubadilishia fedha za kigeni la Rangers Bureau De Change lililopo Magomeni Mapipa, limetoa msaada wa jezi kwa timu ya soka ya Waandishi wa Habari za Michezo nchini (Taswa FC)  kwa ajili ya kuzitumia katika mechi zake mbali mbali za kirafiki na mashindano.
Mkurugenzi Mkuu wa Rangers Bureau De Change na Rangers Tours and Travel Agent, Daudi Madega alikabidhi jezi hizo kwa mwenyekiti wa Taswa FC,  Majuto Omary katika hafla fupi iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo, Magomeni.
Madega alisema kuwa wametoa msaada huo kama mchango wao kwa timu hiyo ambayo inaonyesha mfano kwa kujishughulisha na michezo mbali ya kuandika.
Alisema kuwa Taswa FC imedumu kwa muda mrefu na wao kama wadau wakuu wa michezo nchini, wameamua kuanza na timu hiyo na baadaye kuipa vifaa vya michezo timu yao ya netiboli (Taswa Queens) ambayo ipo katika kiwango cha juu.
“Rangers Bureau De Change na Tours and Travel Agent ni wadau wakuu wa michezo hapa nchini, hii inatokana na mmiliki wake kuwa na timu ya soka (Baker Ranger) ambayo ina historia kubwa katika soka la Tanzania, hivyo msaada huu si wa kubahatisha, tunaahidi kufanya makubwa na timu ikiwa kuwapa mabasi yetu mbali mbali mbali katika safari za timu,” alisema Madega.
Mwenyekiti wa Taswa FC, Majuto Omary aliishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo na kuahidi kuutumia kwa mafanikio ya timu na wala si vinginevyo.

No comments :

Post a Comment