Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, May 22, 2014

Warembo, wadhamini watakiwa Miss Sinza



 Miss Sinza 2013 Prisca Clement katikati mara baada ya kushinda taji la vipaji katika mashindano ya Miss Tanzania 2013
=======  ======  ======
Waandaaji wa mashindano ya kumsaka mrembo wa Sinza, Miss 2014 wametoa wito kwa wasichana wenye vigezo vya kuwania taji la mwaka huu kujitokeza katika mazoezi yanayoendelea kwenye ukumbi wa Meeda Club uliopo katika barabara ya Sinza Mori na Lufungila jijini.

Akizungumza jijini jana, Muandaaji wa mashindano hayo, Majuto Omary alisema kuwa lengo lao ni kuwa na warembo wengi ili kuwapa nafasi majaji kuchagua washindi ambao wataiwakilisha vyema Sinza na vitongoji vyake katika mashindano ya Kanda ya Kinondoni na Miss Tanzania.

Majuto alisema kuwa mpaka sasa jumla ya warembo nane wamejitokeza katika mazoezi ya mwaka huu, idadi ambao haitoshi kutokana na malengo yao ambayo ni warembo 20.

Alisema kuwa uwepo wa washindani wengi, kunatoa changamoto hata kwa majaji na kutoa mrembo bora zaidi na kuwa mwakilishi wa kweli. “Hatujafunga milango ya kuwapokea warembo, tunawaomba wafike mazoezini kuanzia saa 10.30 jioni na kukutana na wakufunzi wetu, Fomu  zinatolewa bure,” alisema Majuto. Majuto pia aliwaomba wadau wa mashindano ya urembo nchini kujitokeza kudhamini mashindano hayo kwa lengo la kuleta maendeleo, kuongeza ushindano mbali ya kutangaza biashara zao.

Alisema kuwa ni fursa pekee kudhamini mashindano hayo kutokana na mvuto uliopo, kwani watazamaji wengi ufika kuangalia mazoezi na wakati wa mashindano.

Taji la Miss Sinza linashikiliwa na Miss Tanzania, Prisca Clement alimaliza katika hatua ya 10 bora katika mashindano ya mwaka jana ya Miss Tanzania na pia alishinda taji la mrembo mwenye kipaji katika mashindano hayo.

No comments :

Post a Comment