Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, December 23, 2009

MAREALLE CUP KUANZA KUUNGURUMA DESEMBA 27

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Executive Solution, Aggrey Marealle (kulia) akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam kuusu Mashindano ya Chifu Marealle yanayotarajia kuzinduliwa Jumapili ya tarehe 27 desemba 2009, kushoto ni Meneja wa Uhusiano wa Kampuni hiyo Ibrahimu Kyaruzi.(Picha na Rajabu Mhamila)
Taasisi ya EABL Foundation chini ya kampuni ya East African Breweries ndiyo itakuwa mdhamini mkuu wa mashindano ya kombe la Chifu Marealle yanayotarajiwa kufanyika Mjini Moshi kuanzia tarehe 27 Desemba 2009 mpaka tarehe 2 Januari 2010.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masuala ya Jamii wa East African Breweries, Bw. Ken Kariuki amesema “Sisi EABL tumedhamiria kuboresha maisha ya watu hapa Afrika Mashariki katika njia endelevu”.
Mashindano haya pia yanatumika kutoa elimu kwa vijana kuhusu mapambano dhidi ya Ukimwi na kuwafundisha vijana jinsi ya kuishi maisha bora. "Tunaamini kuwa mashindano haya yataunganisha watu wa mkoa wa Kilimanjaro na kuweka msingi imara wa vijana na maendeleo ya michezo na kuchangia kutoa elimu kuhusu Ukimwi”, alisema Kariuki.
Mkurugenzi Mkuu wa Executive Solutions, waandaaji wa mashindano hayo Aggrey Marealle alisema zaidi ya timu 14 za soka, timu 7 za netiboli na timu 10 za pool kutoka wilaya za Moshi Mjini, Moshi Vijijini, Siha, Hai na Vunjo zote za mkoa wa Kilimanjaro zinatarajiwa kushiriki kwenye mashindano hayo yanayofanyika kwa mwaka wa tatu. Mashindano hayo yatafanyika katika kata mbalimbali za manispaa ya Moshi kama vile Pasua, Ikulu KDC, Majengo na viwanja vya George Memorial. Fainali zitafanyika katika uwaja wa MUCCOBS siku kumi baada ya uzinduzi. Timu za soka zitakazoshiriki mashindano hayo ni pamoja na Majengo, Bondeni, Lambo FC, Mawenzi , Kiboriloni, Korongoni, Longuo, Miembeni, Rau, Karanga, Kiyungi, Msaranga, Mji Mpya, Pasua, Soweto, Forest, Njoro, Kilimanjaro, Pasua B, Kaloleni, Langasani na Bafana Bafana

No comments :

Post a Comment