Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, December 2, 2009

KILIMANJARO STARS MBABE WA ZANZIBAR HEROES

Timu ya Taifa ya Tanzania Bara maarufu kama Kilimanjaro Stars imeichapa Zanzibar Heroes 1-0 na kufufua matumaini ya kusonga mbele kwenye michuano ya Chalenji inayoendelea nchini Kenya.
Alikuwa ni mshambuliaji Mrisho Ngasa aliyeipa raha Tanzania Bara baada ya kuunganisha pasi ya kiungo anayecheza soka ya kulipwa nchini Norway, Henry Joseph, na kumtungua kwa shuti kali kipa wa Zanzibar, Ally Muhidin, katika dakika ya 18.
Mchezo wote ulitawaliwa na ubabe baina ya wachezaji kiasi hata Kigi Makassi wa Kilimanjaro na kipa wa Zanzibar, Ally Muhidin, walilimwa kadi nyekundu na mwamuzi Thomas Onyango wa Kenya.
Hii ni mara ya pili katika mwaka huu kwa Bara kuishinda Zenji, kufuatia mchezo wao wa michuano hiyo iliyofanyika mwezi Januari nchini Uganda ambapo Bara ilishinda 2-1.
Eritrea na Zimbabwe zilitoka suluhu 0-0 katika mchezo wa Kundi B wa michuano hiyo uliofanyika jijini Nairobi.

No comments :

Post a Comment