Timu ya Taifa ya Tanzania Bara maarufu kama Kilimanjaro Stars imeichapa Zanzibar Heroes 1-0 na kufufua matumaini ya kusonga mbele kwenye michuano ya Chalenji inayoendelea nchini Kenya.
Alikuwa ni mshambuliaji Mrisho Ngasa aliyeipa raha Tanzania Bara baada ya kuunganisha pasi ya kiungo anayecheza soka ya kulipwa nchini Norway, Henry Joseph, na kumtungua kwa shuti kali kipa wa Zanzibar, Ally Muhidin, katika dakika ya 18.
Mchezo wote ulitawaliwa na ubabe baina ya wachezaji kiasi hata Kigi Makassi wa Kilimanjaro na kipa wa Zanzibar, Ally Muhidin, walilimwa kadi nyekundu na mwamuzi Thomas Onyango wa Kenya.
Hii ni mara ya pili katika mwaka huu kwa Bara kuishinda Zenji, kufuatia mchezo wao wa michuano hiyo iliyofanyika mwezi Januari nchini Uganda ambapo Bara ilishinda 2-1.
Eritrea na Zimbabwe zilitoka suluhu 0-0 katika mchezo wa Kundi B wa michuano hiyo uliofanyika jijini Nairobi.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment