Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, May 21, 2012

MISS KIGAMBONI KUPATIKANA JULAI 15



Na Mwandishi Wetu
SHINDANO la kumsaka malkia wa kitongoji cha Kigamboni mwaka huu 'Miss Kigamboni City 2012' limepangwa kufanyika ifikapo June 15 kwenye ukumbi wa Navy Beach ulioko huko Kigamboni hapa jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa shindano hilo, Somoe Ng'itu (pichani) alisema kuwa maandalizi ya kinyang'anyiro hicho yanaendelea na warembo wenye sifa kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini wanaombwa kujitokeza kushiriki.
Mratibu huyo kutoka kampuni ya K& L, alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha shindano la mwaka huu linakuwa bora na kuwapa washiriki watakaokwenda kutwaa taji la Kanda ya Temeke na hatimaye taji la taifa la Redd's Miss Tanzania baadaye mwaka huu.
"Tumeshaanza mchakato wa shindano hili ambalo mwaka huu litakuwa na hadhi ya jiji la Kigamboni, tunawaomba wadau kushiriki kusaidia shindano hili liweze kufanikiwa," alisema Somoe.
Aliongeza kuwa mpaka sasa zaidi ya warembo 12 wameshajiandikisha kuwania taji hilo na wakiwa kambini watakuwa chini ya Hawa Ismail ambaye alikuwa mshindi ya shindano la Kanda ya Temeke mwaka 2003.
Alisema kuwa mazoezi ya shindano hilo yatakuwa yakifanyika kwenye ukumbi wa Brake Point iliyopo Posta jijini ili kutoa nafasi kwa washiriki kuweza kuhudhuria mazoezi hayo.
"Kigamboni ni zaidi ya kitongoji, tunaamini shindano letu litakuwa na mvuto na hadhi ya kipekee kama eneo lake lilivyo," aliongeza.
Alisema kuwa warembo watakaofanya vizuri watapata nafasi ya kuwakilisha kitongoji hicho katika mashindano ya kanda ambayo yatafanyika baadaye mwaka huu.
Aliwataja wadhamini ambao tayari wamethibitisha kudhamini shindano hilo ni pamoja na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Redd's, Dodoma Wine na NSSF.
Salha Israel kutoka Kanda ya Ilala ndiye mrembo anayeshikilia taji la taifa ambapo mwaka huu ratiba ya mashindano hayo imebadilika.

No comments :

Post a Comment