Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, April 15, 2010

CARLOS TEVEZ, WAYNE ROONEY, CESC FABREGAS NA DIDIER DROGBA KUWANIA TUZO YA MWANASOKA BORA WA MWAKA

Carlos Tevez, Wayne Rooney, Cesc Fabregas na Didier Drogba wametajwa kuwania tuzo ya mwanasoka bora wa mwaka inayotolewa na na chama cha wachezaji wa kulipwa (PFA Player of the Year award).

Rooney ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kutwaa tuzo hiyo.

Nyota huyo wa Manchester United amekuwa na wakati mzuri msimu huu, ingawa inaonekana kanakwamba mafanikio ya kusonga mbele katika michuano ya Carling Cup kudoda. Rooney amefunga jumla ya magoli 34 akiwa na klabu yake ya Man United msimu huu katika michuano yote na yeye mwenyewe kkujitaja kuwa ni moja ya wachezaji wenye kipaji Duniani.

Klabu ambayo msimu huu imekuwa tishio katika ligi kuu ya England, Manchester City inawakilishwa na Carlos Tevez, ambaye naye tangu ajiunge na klabu hiyo ni mwenye mafanikio na kufanikiwa kufunga jumla ya magoli 28 katika michuano yote.

Kama Rooney, Nyota wa klabu ya Arsenal Cesc Fabregas amechaguliwa kuwania tuzo mbili ikiwa ni tuzo kuu ya mwanasoka bora na tuzo ya mwanasoka chipukizi wa mwaka.

Ingawa amekuwa akikalia benchi muda mwingi msimu huu akiuguza maumivu, Fabregas amekuwa chachu ya ushindi katika michezo mingi ya klabu hiyo ya washika bunduki.

Wakipewa jina la muda, yaani Mabingwa wateule, Chelsea inawakilishwa na Didier Drogba licha kutofanya vizuri sana kama ilivyokuwa mwaka uliyopita, lakini bado anatajwa kuwa ni mwiba katika lango la wapinzani.

Aston Villa inawakilishwa na James Milner na Birmingham City inawakilishwa Joe Hart ambao wanawania tuzo mwnasoka mdogo pamoja na Rooney na Fabregas

No comments :

Post a Comment