
Nahodha wa Simba Nicodemus Nyagawa (kushoto ) na mlinzi wa timu hiyoJuma Jabu wakishangilia huku wakiwa wambeba Kombe la Ubingwa wa LigiKuu ya Bara mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaamjana.Katika mchezo huo Simba iliicharaza Yanga mabao 4-3. (Picha naMohamed Mambo)
Mbali na ushindi huo Simba ilikuwa inakabidhiwa kombe lake mara baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi kuu ya Vodacom msimu huu bila kufungwa hata mchezo mmoja ambapo imeshinda michezo 19 imedroo miwili na bado ina mchezo mmoja mkononi wa kukamilisha ratiba dhidi ya Mtibwa Sugar ya Manungu Mkoani Morogoro.
Katika mchezo wa jana wachezaji watatu walipewa kadi nyekundu ambao ni Wisdom Ndlovu na Amir Maftaha wa Yanga baada ya kucheza mchezo mbaya dhidi ya wachezaji wa Simba Salm Kanoni na Juma Kaseja wakati Hilary Echesa wa Simba alipewa kadi nyekundu baada ya kuvua jezi alipokuwa akishangilia goli la nne alilofunga dhidi ya Yanga.
No comments :
Post a Comment