Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, April 14, 2010

SBL YAIKABIDHI NGORONGORO HEROES MILIONI 83/


Meneja uhusiano Habari na Mawasiliano wa Serengeti SBL Teddy Mapunda kulia akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Kapteni wa timu ya Vijana Ngorongoro Heroes Himid Mao kwenye ofisi za shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF leo, katikati ni kocha mkuu wa timu hiyo Rodrigo Stokla na mwisho kushoto ni Matadi Yasoda Kaimu mkurugenzi Idara ya Michezo Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo.


Kampuni ya bia ya Serengeti SBL leo imetoa jumla ya shilingi milioni 83 kwa shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF ili kufanikisha maandalizi ya timu ya taifa ya vijana Ngorongoro Heroes chini ya Umri wa miaka 20 katika maandalizi ya safari yao kwa ajili ya mchezo wake na timu ya vijana ya nchini Malawi.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja uhusiano habari na Mawasiliano wa kampuni hiyo Tedd Mapunda amesema katika fedha hizo shilingi milioni 50 ni fedsha taslimu kwa ajili ya masuala ya utawala na shilingi milioni 25 kwa ajili ya kulipia tiketi na shilingi milioni 8 zimetumika kwa ajili ya vifaa vya michezo kwa timu hiyo.

"Kama ambavyo tumekuwa tukisaidia michezo tumeona tuisaidie timu hii ya vijana chini ya miaka 20 kwani tunaamini msaada huu utasaidia kujenga na kuimarisha kikosi bora cha timu ya taifa miaka michache ijayo" amesema Tedy Mapunda.

Ameongeza kuwa tunawatakia Ngorongoro Heroes mafanikio katika mchezo wao huo utakaofanyika katika jiji la Blantyre nchini Malawi na tuna imani kuwa watarudi na ushindi hivyo kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania, Ngorongoro Heroes inatafuta tiketi ya kushiriki kombe la mataifa ya afrika kwa timu za vijana chini ya umri wa miaka 20 katika fainali zinazotarajiwa kupigwa nchini Misri mwaka 2011.

Kampuni ya bia ya Serengeti SBL ni mdhamini mkuu wa timu ya taifa ya mpira wa miguu Taifa Stars kwa miaka kadhaa sasa na chini ya udhamini huo mafanikio ya timu ya taifa yamekuwa yakiongezeka mwaka hadi mwaka hivyo SBL wanastahili kupongezwa kwa udhamini huo.

No comments :

Post a Comment