Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, April 14, 2010

TFF LAWAFUNGIA VIONGOZI, WACHEZAJI LIGI DARAJA LA KWANZA


KAMATI ya Mashindano ya Shirikisho la Soka Tanzania TFF,limewaangushia rungu baadhi ya viongozi na wachezaji wa timu za Daraja la Kwanza kwa utovu wa nidhamu akiwemo Meneja wa Mwanza United, Evarist Hagira ambaye ametozwa faini ya sh. milioni 1 na ushee huku pia akifungiwa miezi sita kujihusisha na michezo.

Kamati hiyo ilikutana Jumamosi jijini Dar es Salaam kujadili mambo mbalimbali yanayohusu ligi daraja la kwanza.

Afisa Habari wa TFF, Frolian Kaijage, amesema baada ya kuitathimini ligi daraja la kwanza waligundua kuna kasoro zilizojitokeza katika baadhi ya michezo ya ligi daraja la kwanza.

Amesema katika mchezo namba 31, kati ya TMK United na Mwanza United, Kocha wa Mwanza United,John Tegete aliwashawishi wachezaji wake kugomea mchezo na kamati imeamua kumfungia miezi mitatu kujihusisha na masuala ya soka.

Amewataja baadhi ya wachezaji wa timu hiyo ambao pia wamekumbwa na rungu hilo la kufungiwa miezi mitatu kujihusisha na soka, kuwa ni pamoja na Hamis Ally, Paulo Joseph, Naftari Matari, Emmanuel Sitta na Othman Othman.

Kaijage amesema mchezo namba tano kati ya Watoto wa A town AFC ya Arusha dhidi ya Mwanza United, mashabiki wa AFC walimfanyia fujo mwamuzi baada ya mpira kumalizika, hivyo nayo AFC imetozwa faini ya Shilingi 150,000.

Ameongeza kuwa mchezo namba 12 kati ya Ruvu Shooting ya Pwani na Coastal Union ya Tanga, waamuzi wa mchezo huo Bamy Bahisha na Mustapha Abdi walichezesha chini ya kiwango, hivyo wamefungiwa miezi mitatu kujihusisha na masuala ya soka.

No comments :

Post a Comment