Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, April 15, 2010

ULINZI YASHIKILIA USUKANI LIGI KUU YA KENYA

Klabu ya ligi kuu ya Kenya Ulinzi Stars na Mathare United ndiyo klabu pekee ambazo hazijapoteza mchezo tangu kuanza kwa msimu wa ligi mapema mwezi Februari.

Hata hivyo klabu hizi mbili zimeachana kwa tofauti kubwa ya pointi ambapo klabu ya Ulinzi inashikilia usukani wa ligi huku Mathare ikishika nafasi ya 5.

IKiwa tayari imechezwa michezo nane hadi sasa katika ligi kuu ya Kenya, Ulinzi Stars inaongoza ikiwa na jumla ya pointi 18, ikiwa ni pointi mbele dhidi ya Tusker FC inayoshika nafsi ya pili.Sofapaka inashika nafasi ya 3 ikiwa na jumla ya pointi 14. Sony Sugar inashika nafasi ya 4 huku ikiwa na point 13 wakati Mathare United ikiwa na pointi 12 ikilala nafasi ya 5 katika msimamo wa ligi.

Gor Mahia inashika nafasi ya 6 ikilingana pointi na klabu ya Mathare United lakini wakitofautiana magoli ya kufunga wakati Nairobi City stars, Western Stima na Sher Karuturi Sports zinashika nafasi ya 7, 8 na 9 zikiwa na pointi 11 kila moja. klabu ya KCB maarufu kwa jina la The Bankers wanahitimisha kumi bora wakishika nafasi ya kumi katika msimamo ikiwa na pointi kumi baada ya michezo ya wikiendi.

Wakati huo huo, Kongowea imefanikiwa kutwaa ubingwa wa kanda ya Pwani katika michuano ya Copa Coca Cola (Coast Province 2010 COPA Coca-Cola) baada ya kuichapa Gede FC 5-4 kwa mikwaju ya penati katika mchezo uliyopigwa katika dimba la Manispaa ya Mombasa.

Kwa upande wasichana, Furaha Ladies inashika nafasi ya kwanza, baada ya kuichapa Mwakitawa Ladies 1-0.

Jijini Nairobi, kipute kilipigwa Posta Grounds ambapo Indomitable FC ilitwa ubingwa wa jumla baada ya kuichapa Korogocho Youth 3-2 kwa mikwaju ya penati wakati wasichana, Dhapks United walitawazwa mabingwa baada ya kuitoa Pioneer Girls kwa goli la ugenini.

mabingwa waliondoka na kitita cha Shilingi za Kenya 30,000 na kila mshindi wa pili aliweka kibindoni Shilingi za Kenya 20,000.

No comments :

Post a Comment