Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, April 13, 2010

ZAIN YAZINDUA MALIPO YA TSHS 1 SAA 24 - "UHURU WA KUONGEA"

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Zain yazindua Malipo ya Tshs 1 saa 24 - "Uhuru wa Kuongea"
.Ongea kwa Tsh 1 kwa sekunde siku nzima.
.Ongea kwa Tsh 1 kwa sekunde kwa dakika usiku kucha.
.Hakuna kujisajili, Hakuna kikomo cha muda, Hakuna Malipo yaliyofichwa, Hakuna kukatika simu hovyo, Hakuna Msongamano wa simu.

Zain, Kampuni inayoheshimika zaidi Tanzani na inayoongoza kwa ubunifu wa bidhaa na huduma, leo imezidi kudhihirisha umahiri wake katika soko kwa kuzindua mpango mpya wa malipo ya kupiga simu yenye viwango vya chini kuliko vyote nchini wa Tsh 1 kwa sekunde unaojulikana kama " Uhuru wa Kuongea".

"Ninayo fuaraha kubwa kuwatangazia kwmaba kuanzia leo wateja wetu waliyopo na wapya katika mpango wa malipo kabla, moja kwa moja watajiunga na mpango wa Ths 1 kwa sekunde saa 24 ikiwa ni pamoja na kuweza kupiga simu kwa kiwango nafuu kuliko vyote cha Tsh 1 kwa dakika baada ya dakika ya kwanza ya Uhuru wa Kuongea wakati wa usikku. Mbali na kutoa ubunifu wa kisasa wa kiteknolojia pamoja na kuwa na huduma bora zenye kuambatana na mtandao kuenea nchi nzima, Zain imejidhatiti kuongoza katika sekta ya mawasiliano kwa kuzidi kutoa viwango nafuu zaidi kwa wateja wetu, na ndiyo maana tumezindua Uhuru wa Kuongea ikiwa ni kutambua mahitaji ya soko la huduma ya simu na kuzingatia unafuu. Hakuna kujisajili, wala gharama za kuhama kutoka mpango mmoja kwenda mwingine, tunaposema "Uhuru wa kuongea" tunamaanisha hicho hicho," Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania Khaled Muhtadi.

Zain imeamua kuwa wazi na bayana, hakuna haja ya kujiunga, wasiwasi wa muda, malipo yaliyofichwa wala simu kukatika katika kutokana na msongamano. Wateja wa Zain wataweza kujivunia Uhuru wa Kuongea kwa urahisi kabisa saa 24 siku zote za wili wakiwa na uhakika wa mtandao madhubuti na ulioenea nchi nzima.

Akiongea na waandishi wa habari wakati wa usinduzi wa mpango huo mpya wa malipo Jijini dar es Salaam, Mkurugenzi wa masoko wa Zain Tanzania Ahsan Syed alisema, "Zain imewekza zaidi ya dola za Marekani milioni 500 katika miundo mbinu ya mawasiliano katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kuhakikisha tunawapa wateja wetu huduma bora ya viwango nafuu popote pale walipo nchini. Mpango wetu wa malipo ya Ths 1 ni rahisi na hauna mkanganyiko wowote na ni kwa saa 24 kwa siku. Muda wa usiku kati ya saa tano usiku hadi saa moja Alfajiri, wateja wa Zain watapiga simu kwa viwango vya chini kabisa kwa Tsh 1 kwa dakika baada ya dakika moja ya kwanza. Wateja wa Zain hawatalazimika kuangalia saa zao za mkononi au ukutani kujua kama wako katika muda wa viwango vya malipo ya Tsh 1, na hii ndiyo inatutofautisha na makampuni mengine."

"Tunatambua kwamba kufanikisha kupatika mawasiliano ni eneo ambalo tunatoa mchango mkubwa kwa jamii na kuchangia kushamiri kwa uchumi wa Tanzania. Simu za mkononi zina mchango mkubwa katika uchumi wetu na ndiyo sababu siyo tu kwamba tunaleta bidhaa zenye ubunifu mkubwa lakini pia tunahakikisha mtandao wetu ni wa kutegemewa na uliyosambaa maeneo mengi zaidi nchini Tanzania. Pia tumesambaza mtandao wetu na bidhaa zetu nchi maeneo mengi vijijini ili kuwawezesha mamilioni ya watu wanaoishi maeneo ya vijijini kuwasiliana na ndugu zao wanaoishi mjini na kuwapunguzia adha mbali mbali zinazosababishwa na umbali. kupitia Uhuru wa Kuongea, Zain inazidi kuwathibitishia wa Tanzania maana halizi ya Ulimwengu maridhawa" Mkurugenzi wa Mtandao wa Zain tanzania Thierry Diasonama alisema.

No comments :

Post a Comment