Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, April 14, 2010

WATANO MBEYA WASHINDA TIKETI Coca-Cola KWENDA KOMBE LA DUNIA AFRIKA KUSINI


Mbeya Aprili 13, 2010... Promosheni ya Kwea Pipa na Coca-Cola inazidi kupamba moto ambapo wateja watano wa Coca-Cola mkoani Mbeya wamebahatika kushinda tiketi kwenda kushuhudia mechi ya fainali ya Kombe la FIFA la Dunia kati ya Brazil na Ureno itakayochezwa kwenye uwanja wa kisasa wa Moses Mabhida jijini Durban Juni 25, 2010.

Fainali za Kombe la FIFA la Dunia zimebeba uzito wa pekee barani Afrika mwaka huu kwa kuwa tamasha hili linalovuta hisia za mamilioni ya wapenzi wa mpira wa miguu duniani linafanyika kwa mara ya kwanza kwenye ardhi ya Afrika tangu kuanzishwa kwake 1930.

Washindi waliotangazwa jijini Mbeya hivi leo ni sehemu ya wateja wa Coca-Cola 200 ambao kampuni hiyo ya vinywaji baridi itawapeleka Afrika kusini kwenda kuungana na maelfu ya wapenzi wengine wa soka kutoka sehemu mbali mbali duniani kusherehekea kombe la dunia.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza washindi hao, Meneja Mauzo wa Coca-Cola Kwanza, Mkoani Mbeya, Bw.Francis Mroso aliwataja washindi hao kuwa ni Deogras L. Kapesa (43) mfanyabiashara wa Mlowo, Mbozi, Tujelimpoki Frank (24), mfanyabiashara kutoka Kyela, Raphael Paul Ngungwi (33), pia mfanyabiashara wa Makunguru, Mbeya.

Wengine in Ally David Kaisi (23) wa Nzovwe, Mbeya ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini na Kelvin Mallya (36) ofisa kutoka Ofisi ya Uhamiaji Tunduma, Mbeya. Waliobahatika kushinda TV aina ya Sony zenye muundo wa kisasa (flat screen) inchi 32 ni Benedicto George, Daniel Kisunga na Petrol Sanga wote wafanyabiashara.

“Tunafurahi kwamba watu wengi wemejitokeza kushiriki promosheni yetu ya Kwea Pipa na Coca-Cola: Shinda tiketi ukasherehekee Kombe la FIFA la Dunia ambayo inawapa fursa adimu Watanzania 200 watakaobahatika kushinda tiketi kwenda kutazama mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia”, alisema Mroso.

Mbali na tiketi za kwenda Afrika Kusini Coca-Cola pia itatoa zawadi mbali mbali kwa wateja 1,200,000 ikiwa ni pamoja na Televisheni ya muundo mpya (flat screen) aina ya Sony, fulana, kofia na soda za bure.

Ili kushiriki, wateja wanatakiwa kununua chupa zenye ujazo wa 300ml au 350ml za Coca-Cola, Sprite au Fanta na kuangalia chini ya kizibo kuona zawadi walizoshinda. Promosheni hii inafanyika katika mikoa yote ya nchi Tanzania hadi Mei 31 na washindi wataendelea kuchukua zawadi zao hadi Juni 15, 2010.

“Napenda kutoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kuburudika na vinywaji vya jamii ya Coca-Cola: Coca-Cola, Fanta au Sprite na kuweka hai matumaini ya kujishindia tiketi za kwenda kutazama mechi ya kusisimua ya kombe la dunia kati ya Brazil na Ureno”,
Alisema Mroso.

Coca-Cola imekuwa mstari wa mbele katika kuwawezesha Watanzania kushuhudia matukio makubwa ya kimichezo. Mwaka jana Coca-Cola iliwawezesha Watanzania kuliona Kombe halisi la FIFA la Dunia kwa mara ya pili baada ya kuliona mara ya kwanza 2006. Coca-Cola pia iliwawezesha Watanzania kuuona laivu Mwenge wa Olympiki 2008 pamoja na kuwa sehemu ya shamra shamra ya Mbio za Mwenge wa Olimpiki ambazo hutangulia michezo ya Olimpiki, ambayo pia ni michezo inayotambaa ulimwenguni kwa umaarufu.

No comments :

Post a Comment