Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, July 8, 2014

AIPS YAANDAA MAFUNZO KWA WANAHABARI CHIPUKIZI



Habari wadau, Chama cha Kimataifa cha Waandishi wa Habari za Michezo (AIPS), kimeandaa mafunzo kwa ajili ya waandishi wa habari za michezo chipukizi wa umri kati ya miaka 19-25 yatakayofanyika Doha Qatar mwishoni mwa mwaka huu wakati wa mashindano ya Dunia ya Mchezo wa Kuogelea.

Kutokana na hali hiyo, AIPS imetoa nafasi chache kwa watakaokidhi vigezo vyao katika mabara mbalimbali duniani. Hivyo nimeattach barua yao na nini kinatakiwa katika mafunzo hayo, ambayo wahusika watagharamia nauli ya kwenda Doha na kurudi mji husika anaotoka mhusika, chakula na malazi muda wote atakaokuwa huko.

Kwa vile hatua ya mwisho itahusisha chama cha nchi husika kumthibitisha muombaji, naomba wote watakaofikiri wana sifa zinazotakiwa wasome vizuri hiyo attachment, kisha watume kwa Makamu Mwenyekiti TASWA, Egbert Mkoko ambaye ndiye atasimamia jambo hilo kwa email: njali5@yahoo.com nataswatz@yahoo.com

Lakini pia kama utamudu unaweza ukaomba binafsi bila kutumia chama na mwisho wa kufanya hivyo ni Agosti 15 mwaka huu na watume kwa email:youngreporters@aipsmedia.com. Kwa watakaotaka kupitia TASWA wajitahidi kabla ya Agosti 10 mwaka huu.

Tusihofie kuomba kwani mwaka 2011 aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mtanzania mwenzetu, Mwita Mwaikenda aliomba nafasi hiyo na aliipata. Ukiwa unahitaji ufafanuzi tuwasiliane 0713-415346.

Nawasilisha,
Katibu Mkuu TASWA

No comments :

Post a Comment