Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, July 10, 2014

JK. AMBARIKI RASMI JANUARY MAKAMBA URAIS 2015


Ampongeza kwa uwezo wake

amsifia kwa uwajibikaji wake

amtakia kila la heri kwenye safari yake. hii hapa sehemu ya maneno ya JK kama yalivyonaswa kutokea BUMBULI



Alichokisema Rais ni hiki Kauli ya JK kama ilivyonaswa akiwa Bumbuli:

 ''January anafanya kazi nzuri ya Ubunge. Pia ananisaidia sana kwa kazi ya Wizara niliyompa. Unajua January alipogombea Ubunge alinificha. Nilikuwa nasikia kwa wenzake tu pale ofisini. 

Baadaye alivyoweka mambo yake sawa ndio akaja kuniambia kwamba Mzee na Mimi najitosa. Nikamtakia heri. Kwa kweli kwa jinsi anavyohangaika na Jimbo lake inaonyesha Ubunge aliutaka Kwa dhati kabisa ya kusaidia watu wa Bumbuli. Nimesikia anafikiria mambo makubwa. Hajaniambia. Mi Nimesikia tu. Namtakia kila la heri. 

Haya mambo anaamua Mungu. Wala hayalazimishwi. Mungu akitaka linakuwa hata kama watu wote hawataki. Mungu akiwa hataki hata kama mtu ukitaka jambo hilo vipi haliwezi kuwa. Mimi nilishauriwa na Mzee mmoja kwamba jambo likifika wakati wake utalipata hata kama utapingwa kiasi gani. Kama halijafika wakati wake haliwezi kutokea. 

Mimi niligombea 1995 sikupata kwasababu haikuwa wakati wake. 2005 ikawa wakati wake nikapata. Na wewe usipopata sasa usiweke nongwa"

No comments :

Post a Comment