Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, August 19, 2009

SIMBA YAWASILI RUVUMA TAYARI KUKIPIGA NA MAJIMAJI

Vijana wa Mtaa wa msimbazi Simba Sports klabu tayari wamewasili Mkoani Ruvuma kucheza mchezo wake dhidi ya wana lizombe Maji Maji ya Songea ikiwa ni mechi ya ufunguzi ya michuano ya ligi kuu Tanzania Bara msimu huu itakayoanza Agasti 23 mwaka huu.
Afisa habari wa kuajiriwa wa klabu ya Simba Cliford Mario Ndimbo amesema kikosi kimeondoka na wachezaji 23 akiwemo kocha mkuu Patrick Phili,Amri Said kocha msaidizi,meneja Innocent Njovu na mkuu wa msafara, Makamu Mwenyekiti Omary Gumbo.
Ndimbo amesema dhumuni la kwenda mapema Songea ni pamoja na kuzoea uwanja ambao umefanyiwa marekebisho na hali ya hewa ya huko kabla ya kuelekea Mbeya kucheza mchezo mwingine na Tanzania Prison.
Akijibu swali kwa nini wachezaji 5 hawakwenda Songea kujiunga na wenzao Ndimbo amesema wachezaji watatu kati ya hao wana matatizo mbalimbali wakiwemo Ramadhani Chombo,Jabir Aziz ambao ni majeruhi.
Ndimbo ametanabaisha kuwa mchezaji Haruna Moshi Boban ameachwa kwa kuwa amefunga ndoa hivi karibuni lakini kwa wachezaji wawili Olimboka Mwakingwe na George Nyanda wameachwa kwa kosa la utovu wa nidhamu.

No comments :

Post a Comment