Wekundu wa Msimbazi Simba imewataka wadau na wapenzi wa mchezo huo kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao dhidi ya Sports Club Villa ya Uganda zitakapochuana katika uwanja wa Uhuru Agasti 8 mwaka huu.
Mwenyekiti wa timu hiyo Hassan Dalali amesema siku hiyo itakuwa siku maalum kwa wana Simba kwani itakuwa ikifanyika kila mwaka na kuzaliwa kwa Klabu hiyo.
Dalali ameongeza kuwa mpambano huo utakuwa na lengo la kuwatambulisha wachezaji wapya waliowasajili kwa wanachama wa Simba na Jezi mpya watakazozitumia katika msimu mpya wa Ligi.
Katika mchezo huo Dalali amesema Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Spika wa Bunge la Jamuhuri ya muungano la Tanzania Mh.Samweli Sitta.
Hata hivyo Dalali amesema kutakuwa na mechi ya ufunguzi kati ya timu ya pili ya Simba chini ya umri wa miaka 20 na Afrika Lyon wenye umri kama huo.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment