Nafasi ya kocha Rafael Benitez siyo swala la kujadili licha klabu ya Liverpool kuondoshwa katika FA Cup baada ya kuchapwa na Reading, taarifa hiyo ni kwa mujibu wa kiongozi wa michezo wa klabu hiyo Christian Purslow.
Benitez anakabiliwa na msukumo mkubwa toka kwa mashabiki hasa baada ya kupteza nafasi kwa klabu hiyo iliyoshuka daraja, kuondolewa mapema katika ligi ya mabingwa na kufanya vibaya katika ligi kuu ya England.
Licha ya matatizo yake, Mhispania huyo bado anaendelea kupambana kubaki katika dimba la Anfield.
hata hvyo katika mahojiano Purslow amesema Benitez anaungwa mkono na uongozi wa bodi ya klabu hiyo.
Kapteni wa zamani wa Liverpoll, Ronnie Whelan jana alikaririwa akisema anaamini kocha Benitez sasa nafasi yake inalazimika kuchukuliwa na kocha mwingine.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment