Timu ya mchezo wa kuogelea imewasili nchini ikitokea jijini Nairobi nchini Kenya ikiwa na ushindi mnono katika mashindano ya kanda ya tatu na ya nne iliyomalizika Jumapili.
Akizungumza na viwanjani.blogspot.com katibu mkuu wa chama cha kuogelea Tanzania TSA, Noel Kiunsi amesema timu hiyo imefanya vizuri na kufanikiwa kurejea na medali tisa katika michuano hiyo.
Lakini wadau sasa hapa najiuliza huko katika mashindano hivi hawa walikuwa wanasema wanatoka wapi? Tanzania kweli? mbona wote wanaonekana ni wazungu! inamaana kweli hakuna mzawa kabisa anayeweza kuogelea? ni kwanini wazawa wenyewe hatushiriki na badala yake nafasi inachukuliwa na wenzetu ambao wengi ukiwauliza utasikia ni watoto wa mabalozi ama wazungu wanaofanya kazi nchini na baada ya muda wanaondoka.Au ndiyo kusema wazazi hawatoi fursa kwa watoto kuogelea? naomba wadau hapo tusemezane.
Hatukatai kuwa wazungu kuwakilisha Tanzania lakini sasa ndiyo timu nzima jamani?
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment