Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, January 14, 2010

VYAMA VYA SOKA MIKOA - RAMADHANI NASIBU BADO TUNAKUHITAJI

Kutoka kushoto Shaibu Nampunde(Lindi) AMin Bkhresa (DRFA) Juma Muruwa (Mtwara) na Joseph Mapunda (Ruvuma).
Mikoa mitano wanachama wa shirikisho la soka Tanzania waemchukulia fomu ya kutetea nafasi ya makamu wa pili wa raisi wa TFF, Ramadhani Nasib.
Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Dar es Salaam DRFA, AMini Bakhresa amesema wamefikia maamuzi hayo ya kumchukulia fomu kwa mapenzi yao kutokana na mchango wa kiongozi huyo tangu achaguliwe kushika nafasi hiyo mwezi Desemba 2008.
Ramadhani Nasibu alilazimika kuacha nafasi hiyo wazi kufuatia, nafasi ya makamu wa pili wa Raisi ambayo huwakilisha vilabu huongozwa na mtu ambaye ni kiongozi wa moja ya klabu zinazoshiriki ligi kuu Tanzania Bara.Mapema Shirikisho la kandanda Tanzania TFF lilitangaza mchakato wa kuziba nafasi zilizoachwa wazi ikiwa ni pamoja na makamu wa pili wa Raisi iliyokuwa ikiongozwa na ramadhani Nasibu ambaye alikuwa kiongozi wa klabu ya Villa Squad ambayo imeshuka daraja, ambapo kwa mujibu wa katiba alilazimika kufanya hivyo.
Wanachama waliyoungana kumchukulia fomu Ramadhani Nasibu ni Mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Dar es Salaam, Amini Bakhresa, Mwenyekiti wa Chama cha soka Ruvuma Joseph Mapunda, Mwenyekiti wa chama cha soka Lindi Shaibu Nampunde, Mwenyekiti wa chama cha soka Tanga Saidi Sudi na Mwenyekiti wa chama cha soka Mtwara Juma Muruwa.
wagombea wengine ambao tayari wamekwishachukua fomu hadi sasa ni pamoja na Mwenyekiti na mkurugenzi wa klabu ya Manyema Abeid Abeid maarufu Falcon.

No comments :

Post a Comment