Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, January 22, 2010

MTIBWA YAINYUKA MANYEMA 5-2

Mabingwa wa michuano ya kombe la Mapinduzi na Ngao ya Hisani Mtibwa Suger leo wamewaadhibu vikali vijana wa Manyema Rangers kwa kuwachabanga jumla ya magoli 5-2.
Alikuwa mchezaji Zuberi Katwila aliyefungua milango ya magoli kwa mtibwa kunako dakika ya saba ya mchezo akiunganisha pasi iliyopigwa na Shaaban Nditi.
Dakika 21 baadae Musa Kipao wa Manyema Rangers alikosa goli la wazi baada ya kipa kuhama golini na kubaki peke yake.
Mnamo dakika ya 35 mchezaji Masoud Ally aliipatia goli la pili Mtibwa Suger akiunganisha mpira wa adhabu ndogo uliyopigwa na Zuberi Katwila.
Kama haitoshi baada ya kurejea kutoka mapumziko ikiwa ni dakika ya 54 Saidi mkopi alifunga goli la tatu akiunganisha mpira uliyopigwa na Omari Matuta huku goli la nne likifungwa na MAsoud Ally kwa shuti la Mbali.
Katika dakika ya 71 Manyema walizinduka toka usingizi na kupata goli la kwanza toka Julias Mrope na kisha dakika ya 79 Mrope tena alifunga, lakini katika dakika ya 84 Yusuph Mrope alipigilia msumari wa tano katika lango la Manyema Rangers.

No comments :

Post a Comment