Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, January 18, 2010

SIMBA YAENDELEZA UBABE KWA MAJIMAJI KATIKA LIGI KUU TANZANIA BARA

Mchezaji wa Simba Ramadhani Chombo akijiandaa kupiga mpira katika mchezo dhidi ya Majimaji uliyochezwa katika uwanja wa Uhuru, Simba ilishinda 2-0.
Timu ya Simba ya jijini Dar es salaam imeichapa timu ya Majimaji kutoka Songea Mkoani Ruvuma magoli 2 kwa Nunge katika mchezo mkali na uliokuwa wa upande mmoja uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru maarufu kama shamba la bibi.
Katika mchezo huo timu ya Simba ndiyo iliyotwala sana mchezo huku wachezaji wake wakikaa na mpira kwa muda mrefu na kufanya mashambulizi ya mara kwamara kwenye lango la timu ya Majimaji, amabpo magoli ya simba yamefungwa na mshambuliaji wake hatari Mussa Hassan Mgosi aliyefunga katika dakika ya 37 kipindi cha kwanza na 72 katika kipindi cha pili hivyo kuifa simba kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya majimaji.
Majimaji walifanya mashabulizi machache katika lango la timu ya Simba ambayo hayakuwa na madhara yoyote langoni mwa Simba hivyo kuwafanya wekundu hao wa msimbazi kuusogelea zaidi ubingwa wa Ligi kuu ya Vodacom 2010 ambao kwa sasa unashikiliwa na timu ya Yanga ya Jijini Dar es salaam.
Simba yenye pointi 36 baada ya ushindi mnono wa leo inahitaji kushinda michezo minne ili iweze kutangaza ubingwa kwa msimu huu wa 2010-2011 kazi ambayo kocha mkuu wa timu hiyo mzambia Patrick Phiri amesema atahakikisha anashinda michezo hiyo ili aweze kutangaza ubingwa mapema zaidi

No comments :

Post a Comment