Shirikisho la kandanda Tanzania TFF limewaomba watanzania wote kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali ikiwemo ya makamu wa pili wa Rais wa Shirikisho hilo.
Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo Fredrick Mwakalebela amesema kwamba fomu za kuwania nafasi hizo zimeanza kutolewa mapema mwezi huu na mwisho utakuwa kesho.
Aidha baada ya wanachama wa klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba kupitisha rasmu ya katiba January 16 na kukubaliana Uchaguzi wa viongozi utafanyika baada ya Ligi Kuu Tanzania Bara Mwakalebela amesema TFF haina shida na hilo chamsingi ni katiba.
wakati huo huo Kamati ya mashindano ya TFF itakutana Jumanne ya tarehe 19 kijadili mambo mbambali ikiwemo ligi daraja la kwanza.
Kamati hiyo ilikutana ijumaa ya wiki iliyopita lakini hawakutoa maamuzi hadi hapo kesho.
Mwakalebela amesema vilabu tisa ndio vitakavyoshiriki ligi hiyo ambapo timu tatu ndizo zitazopanda daraja ambapo mwezi wa tatu ndio ligi hiyo inatakiwa ianze.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment