John Dilinga (DJ JD) akisani mkataba wa kuitumikia Radio Times FM katika kipindi cha BLUST 100.5, anayemtazama ni Meneja vipindi wa Radio Times FM Scholastica Mazula.
DJ mkongwe nchini John Dilinga maarufu DJ JD amesaini leo mkataba na Radio Times FM tayari kuanza kuunguruma kupitia masafa ya 100.5.
DJ JD ambaye inasadikia ndiye mkali na mtundu nchini Tanzania katika kuichezea Dj mashine na uchangaji wa muziki atakuwa akiendesha kipindi cha BLUST 100.5 kila siku kuanzia saa 10:00 jioni hadi saa 1:00 jioni, akitangaza na kumix mziki mwenyewe.
Akizungumza na viwanjani DJ JD amesema kwamba wapenzi wa aina ya uchangaji muziki wake na wasikilizaji wa RAdio Times FM wajiandae kupata burudani ambayo wameikosa kwa muda mrefu.
DJ JD amesema wanaodhani kwamba uwezo wake umeshuka, wafute kabisa mawazo hayo na wakitaka kuthibitisha basi wasikilize Radio Times FM 100.5 na watathibisha kile ambacho wanakifikiria.
DJ JD ni moja ya ma DJ na Watangazaji waliyotoa mchango mkubwa katika kuunyanyua muziki wa kizazi kipya yaani Bongofleva.Hapa John Dilinga (DJ JD) akijadiliana jambo na Meneja Vipindi wa Radio Times FM Scholastica Mazula wakati akisaini mkataba wa kuitumiki Radio Times FM.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment