Wasanii wa Msondo Music band wakiwajibika wakati wa onesho lao lililofanyika Dar es salaam juzi kushoto ni mpiga kinanda Abdul Ridhiwani 'pangamawe' na mpiga gita la Solo Saidi Mabela.(PIcha na Rajabu Mhamila)
moses namuhisa,
Wakati huo huo MWIMBAJI nyota wa muziki wa dansi nchini,Rashidi Mwezingo 'Silver Boy' amesema anaipenda sana bendi ya msondo music hivyo kuwa yupo mbioni kurejea katika kundi la msondo ikiwa ni baada ya wiki kadhaa za kuwa nje kutokana na matatizo ya kiutawala
'Mwezingo amesema mda mchache ujao atalejea kundini na kuanza kuonekana kama mwanzo baada ya kuweka sawa mambo yaliyokuwa yakimkabili ikiwemo ukweli juu ya jukumu walilonalo viongozi wa bendi ya msondo katika kulipa deni analodaiwa na benki ambapo alikopa kupitia udhamini wa TOT.Plus
Lakini nilipohamia Msondo uongozi wa TOT ukauandikia barua uongozi wa msondo kueleza kuwepo kwa deni hilo ambalo napaswa kulipa sh.67,000 kila kila mwezi alisema.
Alifafanua kuwa barua hiyo kwa kiasi flani iliwachanganya viongozi wa Msondo ambapo walidhani jukumu la kulipa deni hilo ni lao, wakati ukweli ni kwamba ninapaswa kulipa mimi kupitia mshahara ninaolipwa kila mwezi.
Alisema badala yake viongozi hawo walisema awawezi kumudu kulipa deni hilo hivyo kuamua kuachana nae, lakini baada ya kuwaelewesha bila shaka wameelewa na sasa yupo mbioni kulejea kundini na kuendelea kutoa burudani jukwaani na nimeshatunga kibaa kitakachokwenda kwa jina la 'heshima ya ndoa' tutakachofanyia mazoezi baada ya kukaa pamoja hivyo kuwataka wapenzi wa Msondo kukaa mkao wa kula
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment