Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, May 10, 2012

CHID BENZI NA DULLY SYKES KUPAGAWISHA CHUO KIKUU UDSM JUMAMOSI HII





 wa muziki wa kizazi kipya nchini Chid Benzi na Dully Sykes wanatarajia kusindikiza mpango wa Indiafrika wa kuunganisha historia ya Utamaduni kati ya Tanzania na India.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mbunifu wa mitindo nchini Mustapha Hasanali alisema mpango huo utahusisha vijana kutoka vyuo vikuu mbalimbali vilivyopo nchini na utafanyika kesho katika ukumbi wa Nkuruma uliopo Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Alisema pia mpango huo  umeunganisha ushirikiano katika masuala ya mitindo kupitia mashindano ya Swahili Fashion Week ambayo yatatoa mshiriki mmoja atakayeiwakilisha nchi kwenye mashindano ya ubunifu ya India fashion week.

Naye Balozi wa India Pinak Chakravarty ambaye pia ni Katibu Maalumu wa idara ya Umma ya Wizara ya Mambo ya Nje na Diplomasia alisema mpango huo utakuza mbinu za ushirikiana wa kimaendeleo baina ya India na nchi za  Afrika.

Chakravarty alisema India na Afrika
inaingia katika ukurasa mpya  wa kihistoria kupitia ukoloni na unyonyaji wa kiuchumi hadi kufikia uhuru.

Alisema uhusiano wa Tanzania na nchi nyingine unazidi kukua kwa kasi na kwamba umeegemea zaidi katika uhusiano wa kiuchumi katika dunia ya utandawazi.

Alisema pia umejikita katika mpango maaalumu wa kibiashara ambao makao makuu yake yako mjini Delhi, na unasimamiwa na idara maalum ya Umma, chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya serikali ya India.

Alisema mpango huo wa Indiafrika ulizinduliwa mwaka 2011 na kwamba mpango hup unakaribisha mbadilishano wa mawazo kati ya vijana kutoka Africa na India kupitia mfululizo wa mashindano mbalimbali ya wajasiriamali, ubunifu na vipaji mbalimbali kwa vijana.

Alisema pia ina lengo la kujenga jukwaa la vijana kutoka India na Afrika lenye nguvu, uvumbuzi na ushindani.

"Kuongezeka kwa uwezo wa ubunifu na kiutamaduni, ni muhimu kwa ajili ya mafanikio, na kuwajenga vijana kuwa raia wazuri wa kimataifa na kukuza ndoto na matarajio yao katika nchi yoyote duniani,"alisema.

Alisema mashindano hayo yatakuwa katika kategoria tatu ambapo kila kategoria washindi watatu watakabidhiwa dola 1000 kila mmoja kutoka kila kanda ambazo ni Afrika Mashariki, magharibi, ya Kati na kusini huku katika fainali itakayowakutanisha washindi wa kanda hizo mshindi atapata dola 10,000.

Alisema washindi hao watapewa ziara ya siku tano itakayoambatana na semina mikutano ya kibiashara itakayokuwa ikifanyika nchini India na katika nchi mbalimbali za Afrika

No comments :

Post a Comment