
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mbunifu wa mitindo nchini Mustapha Hasanali alisema mpango huo utahusisha vijana kutoka vyuo vikuu mbalimbali vilivyopo nchini na utafanyika kesho katika ukumbi wa Nkuruma uliopo Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Alisema pia mpango huo umeunganisha ushirikiano katika masuala ya mitindo kupitia mashindano ya Swahili Fashion Week ambayo yatatoa mshiriki mmoja atakayeiwakilisha nchi kwenye mashindano ya ubunifu ya India fashion week.
Naye Balozi wa India Pinak Chakravarty ambaye pia ni Katibu Maalumu wa idara ya Umma ya Wizara ya Mambo ya Nje na Diplomasia alisema mpango huo utakuza mbinu za ushirikiana wa kimaendeleo baina ya India na nchi za Afrika.

inaingia katika ukurasa mpya wa kihistoria kupitia ukoloni na unyonyaji wa kiuchumi hadi kufikia uhuru.
Alisema uhusiano wa Tanzania na nchi nyingine unazidi kukua kwa kasi na kwamba umeegemea zaidi katika uhusiano wa kiuchumi katika dunia ya utandawazi.
Alisema pia umejikita katika mpango maaalumu wa kibiashara ambao makao makuu yake yako mjini Delhi, na unasimamiwa na idara maalum ya Umma, chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya serikali ya India.
Alisema pia ina lengo la kujenga jukwaa la vijana kutoka India na Afrika lenye nguvu, uvumbuzi na ushindani.
Alisema washindi hao watapewa ziara ya siku tano itakayoambatana na semina mikutano ya kibiashara itakayokuwa ikifanyika nchini India na katika nchi mbalimbali za Afrika
No comments :
Post a Comment