Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, December 5, 2013

muongozaji bora wa filamu,JACK KABIGIRI AFUNGA MWAKA KWA KUWASHUKRU WADAU WA FILAMU.


MUONGOZAJI bora wa filamu Swahiliwood Jackson Kabirigi ‘Jack’ anawashukru wadau wote wa tasnia ya filamu kwa ujumla wake kutokana na mchango wake ambao wamempa kupitia kazi zake ambazo ameshiriki katika kuigiza na kuongoza sambamba na filamu ya Mdundiko iliyomletea sifa baada kuchaguliwa nchini Marekani.

Akiongea na wanahabari msanii huyo ambaye ana sifa za kimataifa amesema kuwa baada ya filamu yake ya Mdundiko kushinda tuzo nje ya nchi na si ndani ya nchi ambapo hata tuzo za ZIFF ilinyimwa, lakini Jack anasema kuwa amejifunza mengi na anatoa shukrani kwa wadau wa filamu ambao wamekuwa bega kwa bega katika kuhakikisha anasonga mbele kisanaa.

“Nawashukru wote wanahabari jamaa zangu hata wale ambao wamekuwa wakinishauri kupitia njia mbalimbali, kila mtu kwangu ana mchango mkubwa sana naheshimu hilo kwa kila mtu kwa nafasi aliyo nayo na kuhakikisha wanafanya jambo kubwa kwa ajili yangu mimi Jack nasema Asanteni sana na Mungu awabariki,”anasema Jack.

Aidha msanii huyo ameamua kuanzisha utaratibu wa kutoa taarifa za maendeleo ya kazi yoyote ambayo atakuwa akiifanya na taarifa kuwafikia wapenzi wa filamu nchini nzima na kuwa ndio njia ya wasanii kujenga mahusiano mema na watazamaji wao ambao kuna wanataka kujua maisha ya wasanii ya kawaida nje ya uigizaji lakini si rahisi.

Jack pia anawashukru sana wapenzi wa filamu Swahiliwood baada ya kuipokea kazi yake vema ya Kisate filamu iliyoingia sokoni hivi karibuni na kufanya vizuri kwa kuteka soko la filamu Bongo, sinema hiyo kaongoza na kuigiza mwenyewe akishirikiana na wasanii wengine wakali kama Tino, Dino, Dennis, Mzee Magari, Hamis Korongo na wasanii wengine wanofanya vizuri.

Msanii huyo ana filamu nyingi sana lakini yeye amechagua filamu kadhaa kuwatambulisha wanahabari na wadau wote kwa ujumla, sinema hizo ni  My Nephew, Money Transfer, filamu hizo kaigizia Afrika ya kusini, Born to Suffer, filamu ya Nunda, The Close, Home village,Ania.

Filamu zingine  ambazo kaingiza na kuzingoza ni Filamu ya Hatia Nguvu ya Imani, CID, Single O, Kigodoro, Kisate na filamu bora ya Mdundiko hizi ni baadhi ya filamu ambazo zote zipo katika ubora wa juu na ameahaidi kufanya mambo makubwa mwaka ujao.

Kazi nzuri ya Jack kutoka Bongo filamu yake aliyoongoza ya Mdundiko kuibuka kama filamu bora iliyofanikiwa katika kipengere cha mafanikio ya hadithi katika filamu (Achievement Narrative in Feature Film) ni ushindi mkubwa kwa mapinduzi ya filamu Bongo Movie. Huyu ndio Jackson Kabirigi muongozaji wa filamu wa Kimataifa 

“NAWAPENDA SANA NAOMBA USHIRIKIANO HUU UENDELEE MIMI NI KIJANA WENU SITOWAANGUSHA KATIKA KULETA MAPINDUZI YA KWELI YA FILAMU TANZANIA MUNGU AWABARIKI NYOTE,” Jackson Kabirigi. 05.December. 2013

No comments :

Post a Comment