Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, May 24, 2013

BFT YAOMBA WADHAMINI



Na Elizabeth John


KOCHA wa timu ya taifa ya ngumi, Remmy Ngabo, ameitaka serikali na wadau wa ngumi nchini, kujitolea kudhamini kambi ya mabondia 16 ambao wanajiandaa na mashindano ya Majiji yanayotarajia kufanyika Julai 1 hadi 7 mwaka huu, jijini Mwanza.
Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika Juni 20 hadi 25, kutokana na kutokuwa na maandalizi ya kutosha, wamelazimika kusogeza mbele tarehe ya kufanyika kwa mashindano hayo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, alisema mabondia hao kwasasa wanaendelea na mazoezi ya kujifua katika uwanja wa Taifa wa Ndani jijini Dar es Salaam kwaajili ya maandalizi ya michuano hiyo.
“Mabondia wapo katika hali ngumu ya maandalizi hivyo wadau wa mchezo huu tunawaomba wajitokeza kudhamini maandalizi haya,” alisema.
Alisema mashindano hayo ya Majiji ni maandaliazi ya kuwaweka sawa mabondia kwaajili ya mashindano ya Afrika na Olimpiki ambayo yanatarajia kufanyika hivi karibuni yakishirikisha mataifa mbalimbali.
“Maandalizi mazuri ya mashindano makubwa ni haya mashindano madogo, mabondia wanatakiwa kufanya mazoezi ya kutosha ili kushiriki mashindano hayo,” alisema Kocha huyo ambaye anatambulika na Shirikisho la Ngumi Duniani (AIBA).

No comments :

Post a Comment