Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, May 27, 2013

Zantel yazindua Epiq Open Mic




Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond na Ney wa Mitego wakitumbuiza jukwaani kwenye uzinduzi wa tamasha la  Epiq Open  Mic 
=======  ======  ========
Katika kuelekea msimu wa sita wa shindano la kuimba la Epiq Bongo Star  Search, kampuni ya simu za mikononi ya Zantel leo imezindua Epiq Open  Mic ikiwa ni nafasi nyingine kwa vijana wenye vipaji vya muziki kuonyesha  vipaji vyao kabla usaili wa Epiq Bongo Star Serach haujaanza.

Epiq  Open  Mic  inatarajiwa  kuwapa  nafasi  vijana  kujifunza  misingi  ya  muziki kutoka kwa mmoja wa watayarishaji wa muziki maarufu zaidi nchini,  Marco Chali. Marco  Chali  ambaye  pia  ni  mtunzi  na  mwimbaji,  ametayarisha  nyimbo  nyngi ambazo zimeshinda tuzo ndani na nje ya nchi za wasanii kama Ms. 

Trinity  kutokea  Jamaica,  A.Y  wa  Tanzania,  Prezzo  wa  Kenya,  J  Martins  kutoka Nigeria na wengine wengi. Tamasha  hilo  la  Epiq  Open  Mic,  ambalo  ni  la  bure  litazinduliwa  rasmi  kwenye  viwanja  vya  Mwembe  Yanga  Temeke  tarehe  26  ya  mwezi  huu  ikisindikizwa  na  wakali  kibao  wa  Bongo  flavor  kama  Diamond  Platnumz,  Madee, Godzila, Ney wa Mitego, Mabeste na Mrap.

Akizungumza  wakati  wa  kuzindua  matamasha  hayo,  Afsa  Biashara  Mkuu wa Zantel, Sajid Khan alisema kampuni ya Zantel inaaminini katika  kuwawezesha vijana kufikia ndoto zao. ‘Muziki ni ajira kwa vijana wengi, na kuamini hilo ndio maana kampuni ya  Zantel  imeamua  kuwafikia  vijana  wote  wenye  vipaji  na  kuwapa  nafasi  ya  kuonekana’ alisema Khan.

Baada  ya  uzinduzi  wa  tamasha  la  Epiq  Open  Mic  Mwembe  Yanga  tamasha  hilo  litaendelea  kila  jumamosi  kwenye  makao  makuu  ya  Zantel  likiwapa nafasi vijana kujisajili na kurekod sauti zao.  Vijana watakaorekodi sauti zao watapigiwa simu na timu ya watayarishaji  wa muziki chini ya Marco Chali pamoja na wanamuziki ili kuwapa ushauri   wa namna ya kuboresha muziki wao zaidi. 

‘Zantel imejipanga kutumia fursa hii kuwahamasisha vijana kushiriki katika  kukuza  vipaji  vyao,  kuongeza  uelewa  wa  mambo  ya  muziki  pamoja  na  kuchangamkia fursa zilizopo katika muziki’ alisisitiza Khan. Epiq  Open  Mic  pia  inatarajia  kuwapa  fursa  ya  kurekodi  baadhi  ya  vijana  watakaokua na vipaji.

No comments :

Post a Comment