Bondia Awadhi Tamimu kushoto akipambana na bondia wa Nchini Urusi aliyemtaja kwa jina la Bokt kulia.
Bingwa wa ngumi za kulipwa ashrafu Suleimani imetamba kumdunda mpinzani wake Awadh Tamim katika pambano la kuwania ubigwa wa Afrika wa mchezo huo mchezo utakaofanyika July 18 katika ukimbi wa DDC Mlimani jijini Dar es Salaam.
Akichonga na kipindi michezo ya Radio Times FM Ashrafu amesema amejiandaa vizuri katika pambano hilo ambalo litaonyesha historia yake katika mchezo huo.
Ashrafu amesema kwamba ana hofu na mchezaji huyo na uhakika wa kupiga upo kutokana na maandalizi makali anayoyafanya.
Ashrafu amefikia uamuzi wa kuzichapa na Awadhi Tamimu baada ya Bodnia huyo kamua kuacha wazi mikanda yake ya Ubingwa wa Tanzania na Afrika Mashariki kufuatia kukosa mpinzani hapa nchini.
Awadhi Tamimu amesema kwa muda mrefu amekuwa na kiu ya kuwa bingwa wa Afrika na kusaka mataji makubwa ya Dunia katika uzito wa juu, lakini amekuwa akikosa mpinzani hapa nchini, hivyo amefikia maamuzi ya kuacha wazi mikanda hiyo ili awanie ubingwa wa Afrika.
Promota wa pambano hilo Shomari Kimbau amesema Bingwa wa Pambano hilo kati ya Awadhi Tamimu na Ashrafu Suleiman ndiyo atawania ubingwa wa Afrika.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment