Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, July 13, 2009

UJIO WA PHIRI SIMBA BADO KITENDAWILI

Kitendawili cha kocha mkuu wa Simba Ptrick Phiri lini atarejea Tanzania baada ya kukwama Zambia alipokwenda katika mapumziko bado kigumu.

Akizungumza na Viwanjani.blogspot meneja wa timu ya Simba Innocent Njovu amesema kocha Phiri anaweza kuwasili mwishoni wiki hii.

Kauli hii inapingana na ile iliyotolewa jana na uongozi wa klabu ya Simba kwamba kocha huyo anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania siku ya Jumanne.

"Kocha Phiri tunamtegemea kuwasili Tanzania tayari kwa maandalizi ya ligi kuu Tanzania bara mwishoni mwa juma hili" amesema Njovu

Njovu amesema kufuatia kuchelewa kwa Phiri kumepelekea timu kusita kuingia kambini sasa kwa juma la pili tangu iarifiwe itaanza kambi hapo Julai mosi.

"timu haiwezi kuingia kambini hadi kocha mkuu atakapowasili nchini" amesema Njovu na kudai "kwa sasa timu inafanya mazoezi ya kawaida ikiwa chini ya kocha msaidizi"

Patrick Phiri kocha mkuu wa klabu ya Simba alikwa nchini Zambia baada ya kufiwa na kaka yake, lakini baadae gazeti moja la Zambia likaandika kocha huyo wa wekundu wa Msimbazi ameshindwa kesi ya madai ya umiliki wa nyumba yake jambo lilidaiwa kumchelewesha.

1 comment :

  1. Timu ya Mazembe ya Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo imeelekea Tunisia kupambana nyota wa sahel katika Michuano Caf.

    ReplyDelete