Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, July 15, 2009

SIMBA SASA YAPUMUA !


Kocha Phiri mwenye suti na tai katikati ya mashabiki wa SIMBA!

KOCHA Mkuu wa klabu ya Simba, Mzambia Patrick Phiri amewasili nchini siku ya Jumatano jioni na kupewa mapokezi makubwa na wanachama huku akisindikizwa na vikundi vya ngoma vya klabu hiyo maarufu Mpira Pesa.

Kocha huyo baada ya kuwasili, alipanda basi dogo la klabu hiyo, huku akiambatana na Mwenyekiti wa klabu hiyo, Field Masho Hassan Dalali na Meneja wa timu, Innocent Njovu bila ya mchezaji yoyote kama ilivyodaiwa awali na uongozi wa klabu hiyo.

Hiyo imekuwa ni faraja kubwa kwa Simba ambao walijawa na hofu ya kocha huyo kuingia mitini kama ilivyowahi kutokea siku za nyuma wakati timu hiyo ilipokuwa ikikabiliwa na michuano.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili nchini kwa ndege ya Shirikika la Ndege la Zambia majira ya saa 10 jioni, Phiri alisema, ameyapokea mapokezi hayo kwa mshtuko mkubwa kwani hakutegemea kupokewa hivyo.

Amesema kuchelewa kwake kufika nchini si kwamba alifanya makusudi, bali ni matatizo yaliyokuwa yakimkabili kwao na ilikuwa ukizingatia ilimharibia mipango yake.

No comments :

Post a Comment