Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, July 16, 2009

Wanawake wa Afrika wadhihirisha umwamba Uholanzi

Timu ya taifa ya wanawake ya Afrika Kusini Banyana Banyana!!!

Timu ya taifa ya wanawake ya Afrika Kusini imefanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya timu ya taifa ya wanawake ya Switzerland katika mchezo wa fainali uliyoshirikisha mataifa manne nchini Uholanzi.
Mchezaji soka bora wa kike wa Mwaka wa Afrika Noko Matlou, Mamphashe Popela na Janine Van Wyk walifunga magoli na kuipa ushindi Afrika Kusini.
Meneja wa kikosi hicho Fran Hilton-Smith amesema anajisikia fahari sana vijana kuibuka na ushindi.
Naye kocha Augustine Makalane amesema ni kikosi ambacho bado anakijenga lakini wamefanya vizuri kutokana na kile ambacho wamejifunza mara ya mwisho walipokuwa Cyprus.
Banyana Banyana walianza michuano hiyo vibaya, kwa kuchapwa 5-0 na China katika mchezo wa ufunguzi.
kapteni wa kikosi hicho Kylie Anne Lowe amesema kwamba pipingo walichokipata dhidi ya China kiliongeza chachu ya kufanya vizuri kwa kikosi hicho ambacho kilikuwa hakina uzoefu wa michuano ya kimataifa.
Katika mchezo wa pili iliibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Uholanzi, huku magoli yakifungwa na Lebogang Thobejane na Popela.
Wa Afrika Kusini waliyopo Uholanzi waliunganisha pamoja na kuishangilia Banyana Banyana, na kudai hizo ni salamu za michuano ya Dunia 2010.

No comments :

Post a Comment