Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, July 13, 2009

SAFARI YA BONDIA AWADHI TAMIMU KUWANIA UBINGWA WA AFRIKA YAINGIA MDUDU

Maandalizi ya pambano la ngumi za kulipwa la kuwania ubigwa Afrika kwa Awadh Tamim dhidi ya bondia Ashrafu Suleiman pambano litakalopigwa katika ukumbi wa DDC mlimani jijini Dar es Salaam yamekamilika.

Akiongea na kipindi cha michezoi cha Radio Times FM mwandaaji wa pambano hilo Shomari Kimbau amesema kwamba pambano hilo linatakuwa upinzania wa hali ya juu kutokana na maandalizi kabambe yanayofanywa na mabondia hao.

Amesema sababu kubwa ya pambano hilo ni baada ya Awadhi Tamimu kutangaza kuacha wazi mikanda yake ya Ubingwa wa Tanzania na Afrika Mashariki na kuweka nia ya kuwania ubingwa wa Afrika lakini bondia Ashrafu Suleimani akataka wapambane ili kumuonesha kwamba kunamabondia wanauwezo.

Awadhi Tamimu alifikia maamuzi hayo ya kuachia mikanda hiyo wazi baada ya kukosa mpinzani, hivyo Ashrafu amesema anataka kumuonyesha kwamba anaweza.

Kimbau amesema Bingwa atakayepatikana katika pambano hilo ndiyo atakayecheza pambano la kuwania ubingwa wa Afrika baada ya kutwaa ubingwa wa Tanzania katika uzito wa juu.

No comments :

Post a Comment