Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, July 15, 2009

Tabora uso kwa uso na Mji Magharibi fainali ya Copa Coca Cola


TIMU ya Mkoa wa Tabora imekata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 baada ya kuifunga Morogoro bao 2-1 katika mchezo wa nusu fainali uliofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Tabora walikuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza dakika ya 10 kupitia kwa mshambuliaji wake, Said Khalfani aliyefunga kwa shuti kali baada ya kupokea pasi kutoka Lameck Simoni.

Moro walisawazisha bao hilo dakika 47, kupitia kwa Kulwa Salanga kwa shuti kali akiwa ndani ya eneo la hatari na mpira kutinga wavuni.

Bao hilo liliwaongezea nguvu Tabora na kuongeza mashambulizi langoni mwa wapinzani wao, dakika ya 76, Issa Swedy aliifungia timu yake bao la pili kwa kichwa baada ya kuunganisha mpira wa kona uliopigwa na Hussein Moshi.

Kwa matokeo hayo, Tabora itakutana na Mjini Magharibi katika mchezo wa fainali itakayochezwa Uwanja wa Uhuru, Jumamosi huku Morogoro wakikutana na Kigoma kutafuta mshindi wa tatu.

No comments :

Post a Comment