Timu ya soka ya Manyema FC ya jijini Dar es Salaam leo imewasilisha majina ya wachezaji waliowasajili kuchezea ligi kuu Tanzania Bara msimu ujao.
Akiongea na viwanjani Mkrugenzi Mtendaji wa Manyema FC Ally Mmanga amesema wachezaji wote waliowasajili msimu huu ni wa ndani ya nchi na si nje ya nnchi.
Amesema wamesajili jumla ya wachezaji 28 huku akismea wachezaji 16 ni wa zamani na wachezaji 12 ni wachezaji wapya.
Amewataja baadhi ya wachezaji kuwa ni pamoja na goligipa Odo Nombo Mulemba toka Kagera, Amoa Kefa Zulu, Abrahamu Masunga, Musa Kipao na Steve Mkuchika.
Mmanga amesema swala la Katibu wa kuajiriwa bado wanalifanyia kazi na litakapokuwa tayari wataliweka hadharani.
Kuhusu maandalizi ya ligi kuu Tanzania bara msimu ujao, amesema tarehe 1 mwezi wa nane wataweka kambi nje ya Dar es Salaam.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment