Golikipa wa klabu ya Newcastle Steve harper amedai klabu hiyo inakufa taratibu, kifo cha maumivu huku mmiliki Mike Ashley akijaribu kuiuza klabu hiyo bila mafanikio.
Wanunuzi kadhaa wamekuwa wakitangaza nia yao ya kutaka kuinunua kabla ya kushuka daraja na baada ya kushuka daraja lakini wamekuwa hawafikii makubaliano na hatimaye kupotea kusiko julikana.
hatua hiyo imemuacha Alan Shearer njia panda asijue lini atasaini mkataba wa kuinoa timu hiyo, huku wachezaji nao wakiwa katika giza totoro lisilo hata lepe la mwanga la kuwaonyesha njia.
Harper akizungumza kwa uchungu amesema inauma sana inapofika wakati mtu unakuwa hujui nini cha kufanya, huku wachezaji nao wakijua bosi wao maji yamemfika shingoni, licha ya kuwa na ndoto za Alinacha kwamba siku moja watajenga nyumba angani na kuwa matawi ya juu.
Amesema kila moja, mashabiki, wachezaji, uongozi wanataka kuijenga upya klabu hiyo lakini hali ndiyo inazidi kuwa ngumu kila kukicha.
RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ATOA MKONO WA EID KWA WENYE UHITAJI DODOMA
-
Mkuu Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule Machi 30,2025 amekabidhi kwa
niaba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia
Suh...
3 hours ago
No comments :
Post a Comment