Golikipa wa klabu ya Newcastle Steve harper amedai klabu hiyo inakufa taratibu, kifo cha maumivu huku mmiliki Mike Ashley akijaribu kuiuza klabu hiyo bila mafanikio.
Wanunuzi kadhaa wamekuwa wakitangaza nia yao ya kutaka kuinunua kabla ya kushuka daraja na baada ya kushuka daraja lakini wamekuwa hawafikii makubaliano na hatimaye kupotea kusiko julikana.
hatua hiyo imemuacha Alan Shearer njia panda asijue lini atasaini mkataba wa kuinoa timu hiyo, huku wachezaji nao wakiwa katika giza totoro lisilo hata lepe la mwanga la kuwaonyesha njia.
Harper akizungumza kwa uchungu amesema inauma sana inapofika wakati mtu unakuwa hujui nini cha kufanya, huku wachezaji nao wakijua bosi wao maji yamemfika shingoni, licha ya kuwa na ndoto za Alinacha kwamba siku moja watajenga nyumba angani na kuwa matawi ya juu.
Amesema kila moja, mashabiki, wachezaji, uongozi wanataka kuijenga upya klabu hiyo lakini hali ndiyo inazidi kuwa ngumu kila kukicha.
MAKALLA,LAIZER WAZINADI FURSA ZA UTALII NA UWEKEZAJI NGORONGORO
-
Naibu Kamishna wa Uhifadhi, Huduma za Shirika Ngorongoro Bw. Aidan Makalla
(kulia) akiwa ameambatana na Abdiel Laizer Afisa Utalii Mkuu Msaidizi
amekutan...
3 hours ago
No comments :
Post a Comment