Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, July 19, 2009

Mjini Magharibi watwaa ubingwa wa michuano ya Copa Coca Cola U -17

TIMU ya Mijini Magharibi jana iliibuka bingwa wa mpya wa michuano ya Vijana chini ya miaka 17 'Copa Coca Cola' baada ya kuichapa Tabora bao 2-1 katika mchezo wa fainali uliochezwa katika uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Mchezo huo uliochezwa katika dakika 120 baada ya dakika 90 kwisha kwa sare ya mabao 1-1, hivyo mwamuzi wa mchezo huo kuongeza dakika 30 za nyongeza.

Kutokana na matokeo hayo Mjini Magahribi wamejinyakulia kitita sh. milioni 4.5 wakati nafasi ya pili imekwenda kwa Taborea wataoboka na sh. milioni tatu wakati timu ya Morogoro itapata sh milioni mbili baada ya kushika nafasi ta tatu baada ya kuinyuka Kigoma kwa bao 1-0.

Mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani katika dakika zote za mchezo lakini Majini Magharibi ndio walionekana kutawala mpira kwa muda mrefu.

Pamoja Mjini Magharibi kutawala mchezo huo lakini iliwabidi kusubili hadi kipindi cha pili kupata bao hilo dakika ya 67 mfungajji akiwa Ibrahimu Rajabu kwa shuti kali la mbali lililomshinda kipa wa Tabora.

Baada ya Tabora kufungwa bao hilo waliongeza kasi ya mchezo na kufanikiwa kupata bao kusawazisha dakika ya 90 mfungaji akiwa Lameck Simon na kufanya mchezo huo kuongezwa dakika za nyongeza.

Mjini Magharibi walipata bao la pili dakika ya 93 mfungaji akiwa Mohamed Abdulrahim baada ya kupasua ngome ya Tabora na kuachia shuti kali.

Mgeni rasmi katika mchezo huo alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mrisho Kikwete na alikabidha kombe kwa mshindo wa michuano hiyo.

No comments :

Post a Comment