Mchezaji Michael Owen amefanikiwa kufunga goli katika mchezo wake wa kwanza akiwa na Manchester United huku akifunga goli la ushindi katika mchezo dhidi ya kikosi cha kwanza cha timu ya taifa ya Malaysia na kuichapa 3-2 katika mchezo uliyochezwa Kuala Lumpur.
Wayne Rooney na Nani ndiyo walikuwa wa kwanza kupta magoli ya ushindi kwa mabingwa hao wa England, huku mchezaji Amri Yahyah akifunga magoli mawili ya Malaysia kabla ya Owen kuingia akitokea benchi na kufunga goli la ushindi.
Hata hivyo baada ya kutokea matukio ya ugaidi huko Jakarta kumeilazimisha klabu ya Manchester United kuahirisha safari ya kwenda Indonesia na kujikuta ikiathiri ziara yao ya nchi za mashariki ya mbali.
Ingawa Rooney alitolewa nje kutibiwa baada ya kuumizwa na mlinzi wa klabu ya Malaysia.
Rooney aliweza kurejea uwanjani na kufanikiwa kuipangua ngome ya ulinzi ya Malaysian na pasi iliyopigwa na Dimitar Berbatov ambayo iliwaparaza mabeki na kumkuta Rooney aliuweka mpira wavuni.
Dakika 20 baadae mshambuliaji wa kimataiaf wa Ureno Nani alifunga goli la pili na matokeo kuwa 2-0 kabla ya Malysia kusawazisha.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment